Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/08 uku. 8
  • Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Matangulizi Yenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Pata Manufaa za Kitabu Reasoning
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Tumia Kikamili Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Tumia Kitabu Reasoning Katika Sehemu Zote za Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 12/08 uku. 8

Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?

1. Mtume Paulo na Yesu waliwafundishaje wengine?

1 Mtume Paulo alijitahidi ‘kujadiliana kwa kutumia Maandiko.’ (Mdo. 17:2, 3; 18:19) Kwa kufanya hivyo, alimwiga Yesu, ambaye alinukuu Maandiko mara nyingi na kutumia mifano kuwasaidia wasikilizaji wake waelewe mapenzi ya Mungu. (Mt. 12:1-12) Kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kimekusudiwa kutusaidia kufanya vivyo hivyo.

2. Tunaweza kutumiaje kitabu Kutoa Sababu kutayarisha tangulizi zenye matokeo?

2 Kutayarisha Tangulizi Zenye Matokeo: Katika ukurasa wa 9-15, kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kina tangulizi zinazowachochea watu wapendezwe. Kujifunza tangulizi mbalimbali na kuzitumia, hasa ikiwa unahubiri eneo mara nyingi, kutafanya huduma yako ipendeze na kukusaidia kubadilika kulingana na hali na kuanzisha mazungumzo kwa urahisi. Unaweza kusoma tangulizi hizo moja kwa moja katika kitabu unapohubiri kwa simu au unapotumia kifaa cha mawasiliano mahali penye nyumba zenye ulinzi mkali.

3. Ni habari gani zilizo katika ukurasa wa 16-24 wa kitabu Kutoa Sababu zitakazotusaidia katika huduma?

3 Kushinda Vizuia-Mazungumzo: Unaweza kufikiria vizuia-mazungumzo vinavyoweza kutokezwa katika eneo lenu na kutumia dakika chache kabla ya mahubiri kuchunguza ukurasa wa 16-21 ili uone jibu unaloweza kutoa. Je, huenda wenye nyumba fulani ni Wabudha, Wahindu, Wayahudi, au Waislamu? Ikiwa ndivyo, habari zilizo katika ukurasa wa 21-24 zitakusaidia.

4. Tunaweza kutumiaje kitabu Kutoa Sababu wakati swali linapozuka au habari inayoweza kuleta mabishano inapozushwa?

4 Kujibu Maswali: Kitabu Kutoa Sababu kinaweza kutusaidia pia wakati swali linapozuka au habari fulani inayoweza kuleta mabishano inapozushwa. Unaweza kumweleza tu mtu huyo kwamba ungependa kumwonyesha jambo fulani lenye kupendeza kuhusu habari hiyo kisha utoe kitabu Kutoa Sababu. Kwa kuwa habari zimeorodheshwa katika mpangilio wa alfabeti, chunguza kichwa kikuu ambacho unafikiri kitakuwa na habari unayohitaji. Kisha tazama maswali yaliyoandikwa kwa herufi nzito. Usipopata haraka habari unayotafuta, fungua fahirisi iliyo nyuma. Ukipata habari inayofaa, isome moja kwa moja katika kitabu hicho. Ikiwa unazungumzia andiko hususa, unaweza kupata habari unayohitaji katika ukurasa wa 445 chini ya kichwa “Maandiko Ambayo Mara Nyingi Hutumiwa Kimakosa.”

5. Kitabu Kutoa Sababu kina faida gani nyingine?

5 Matumizi Mengine: Wengine huwa na nakala ya kitabu Kutoa Sababu kazini au shuleni ili kiwasaidie kujibu maswali kama vile, ‘Kwa nini hamsherehekei sikukuu?’ Vijana wameona habari zilizo chini vya vichwa “Uumbaji” na “Mageuzi” kuwa muhimu wanapotayarisha ripoti za shule. Je, utamtembelea mtu ambaye ni mgonjwa au aliyepoteza mpendwa wake katika kifo? Habari zilizo chini ya kichwa “Kitia-Moyo” zinaweza kukusaidia kutoa faraja ya Kimaandiko. Kitabu Kutoa Sababu kina habari muhimu pia kwa ajili ya wale wanaotayarisha hotuba na wale wanaoongoza mikutano ya utumishi wa shambani.

6. Lengo letu ni nini tunapohubiri?

6 Tunapohubiri, lengo letu si kushinda mabishano; wala si kuwasilisha habari tu. Tunataka kujadiliana kwa ustadi tukitumia Maandiko. Tunapotumia vizuri kitabu Kutoa Sababu, tunaonyesha kwamba tunaangalia daima kufundisha kwetu.—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki