Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 29, 2008. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 20 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Novemba 3 hadi Desemba 29, 2008.
SIFA ZA USEMI
1. Kwa nini ni muhimu kutoa himizo “kwa msingi wa upendo”? (Flm. 9) [be uku. 266 fu. 2-4]
2. Tunaweza kuwatiaje moyo wengine? [be uku. 268 fu. 4–uku. 269 fu. 2]
HOTUBA NA. 1
3. Barua ya Paulo kwa Tito ina mambo “mazuri na yenye faida” kwetu leo jinsi gani? (Tito 3:8) [si uku. 241 fu. 8]
4. Kwa nini barua ya kwanza ya Petro ilikuwa ya wakati unaofaa? [si uku. 251 fu. 1]
5. Tunapaswa kuhisije kuhusu vifananisho vya Ufunuo? [si uku. 263 fu. 1]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
6. Kwa nini huenda Paulo alihusianisha ‘kutokuwa wachongezi’ na ‘kutokuwa watumwa wa divai nyingi sana’ katika Tito 2:3? [w94 6/15 uku. 20 fu. 12]
7. Kwa kuwa Shetani ana “uwezo wa kusababisha kifo,” je, inamaanisha kwamba anaweza kusababisha kifo cha mapema cha mtu yeyote yule? (Ebr. 2:14) [w08 10/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Tito, kwa Filemoni, na kwa Waebrania”]
8. Ni nani “yule mwanadamu mwenye kufanya agano” wa agano jipya? (Ebr. 9:16) [w08 10/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Tito, kwa Filemoni, na kwa Waebrania”]
9. Inamaanisha nini kuwa mwenye amani, na tunaweza kujiuliza maswali gani kuhusiana na hilo? (Yak. 3:17) [w08 3/15 uku. 24 fu. 18]
10. Maneno “Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu” yanamaanisha nini? (1 Yoh. 3:20) [w05 8/1 uku. 30 fu. 19]