Matangazo
◼ Toleo la vichapo la mwezi wa Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Watu wakisema kwamba wana watoto, waonyeshe kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa wenye nyumba tayari wana kitabu hicho, wahubiri wanaweza kutoa kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kwenye karatasi zinazochujuka au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1992. Februari: Toa kitabu kimoja kati ya vifuatavyo, ikiwa vinapatikana, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidini sana kuanzisha Mafunzo ya Biblia.