Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/00 uku. 8
  • Jinsi ya Kusitawisha Uwezo wa Kutoa Sababu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kusitawisha Uwezo wa Kutoa Sababu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Tumia Kikamili Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Tumia Kitabu Reasoning Katika Sehemu Zote za Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Pata Manufaa za Kitabu Reasoning
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 2/00 uku. 8

Jinsi ya Kusitawisha Uwezo wa Kutoa Sababu

1 Ufafanuzi mmoja wa neno “sababu” ni “kuongea na mtu mwingine ili kuathiri matendo au maoni yake.” Ili kuongeza ubora wa matokeo katika huduma, wahitaji kusitawisha uwezo wa kutoa sababu na wale unaokutana nao. (Mdo. 17:2-4) Lakini waweza kusitawishaje ustadi huu?

2 Huanza kwa Kutafakari: Unapojifunza kweli za Biblia, utaona likiwa jambo lenye msaada kutafakari habari hiyo. Sehemu za habari hiyo zikionekana kuwa ngumu zaidi, chukua wakati ufanye utafiti na kutafakari majibu yake. Jaribu kuelewa waziwazi si maelezo yaliyotolewa tu bali pia sababu za Kimaandiko za maelezo hayo.

3 Utayarishaji kwa Ajili ya Huduma Wahusika: Fikiria jinsi ambavyo ungeeleza kweli kwa watu wa aina mbalimbali. Tokeza swali lenye kuamsha fikira ili kuchochea upendezi. Amua jinsi ya kuingiza hoja ya Kimaandiko na utoe sababu juu yake. Tazamia vipingamizi ambavyo huenda vikatokezwa, na ufikiri jinsi ya kuvizungumzia. Kazia katika kichapo kinachotolewa jambo kuu litakalotumiwa vizuri.

4 Fuata Kielelezo cha Yesu: Yesu aliweka kigezo bora zaidi cha kutoa sababu kwa matokeo katika Maandiko. Ili uchanganue jinsi alivyofundisha, fikiria simulizi linalopatikana katika Luka 10:25-37. Angalia utaratibu huu: (1) Elekeza fikira kwenye Maandiko unapojibu maswali ya watu. (2) Waombe watoe maelezo, na uwapongeze wanapotoa maelezo yenye ufahamu. (3) Hakikisha kwamba uhusiano kati ya swali na Maandiko wakaziwa. (4) Tumia kielezi kinachogusa moyo ili kuhakikisha kwamba maana halisi ya jibu inaeleweka.—Ona Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1986, ukurasa wa 22-23, fungu la 8-10.

5 Tumia Chombo Tulichopewa: Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kilichapishwa kuwa kitabu kinachoweza kubebeka cha huduma. Utangulizi wake mbalimbali, majibu yake kwa yanayotazamiwa kuwa vizuia mazungumzo, na hoja zenye kusababu hutusaidia kusitawisha uwezo wa kutoa sababu. Kitabu Kutoa Sababu ni chombo chenye thamani ambacho twapaswa kukibeba sikuzote tukiwa katika utumishi wa shambani na tusisite kukitumia tunapokuwa na mazungumzo ya Biblia. Chunguza ukurasa wa 7-8 wa kitabu hicho uone jinsi unavyoweza kukitumia kwa manufaa kubwa.

6 Kusitawisha uwezo wa kutoa sababu kutazidisha ubora wa ustadi wako katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Hilo litatokeza baraka tele kwako na kwa wale unaokutana nao hudumani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki