Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/98 uku. 8
  • Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na Kiu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na Kiu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Madokezo ya Utoaji wa Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Mtegemee Yehova Akuze Vitu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 2/98 uku. 8

Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na Kiu

1 Kama ilivyotabiriwa na nabii Amosi, familia ya kibinadamu leo yateseka kwa ‘kiu si ya maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya BWANA.’ (Amo. 8:11) Ili kusaidia watu walio katika hali hii ya kukauka ya kiroho, twawaambia kuhusu maandalizi ya Mungu ya kuwakomboa wanadamu watiifu kutoka katika dhambi na kifo, yanayofafanuliwa katika sura ya mwisho ya Ufunuo kuwa “mto wa maji ya uhai.” Tuna pendeleo la kutoa mwaliko kwa kila mtu aliye na kiu ya kupata uadilifu aje “achukue maji ya uhai bure.” (Ufu. 22:1, 17) Twaweza kufanyaje hivyo wakati wa Februari? Kwa kuwatolea wanaopendezwa kikweli kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Huenda ukataka kujaribu utoaji huu mbalimbali:

2 Kwa kuwa watu wengi wanahangaishwa na mambo ya kiafya, huenda ukaona mfikio huu kuwa wenye matokeo:

◼ “Wengi wanahangaishwa na gharama yenye kuongezeka ya utunzaji wa afya ulio bora. Labda umewaza kwa kiasi fulani kuhusu jambo hilo. [Ruhusu itikio.] Je, kuna utatuzi wa kudumu wa tatizo hili? [Ngojea itikio.] Hapa pana tazamio la ajabu sana.” Soma Ufunuo 22:1, 2. Kisha fungua kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye picha iliyo kwenye ukurasa wa 308-309, na utumie fungu la 22 kwenye ukurasa wa 311 kuieleza. Malizia kwa kusema: “Kichapo hiki huzungumzia kila mstari katika Ufunuo.” Mwenye nyumba akionyesha kupendezwa kikweli, toa kitabu hicho kwa mchango ulioagizwa. Fanya mipango ya kurudi.

3 Unapofanya ziara ya kurudia, ungeweza kuanza upya mazungumzo yenu kwa kusema:

◼ “Wakati uliopita nilipokuwa hapa, tuliongea kuhusu utatuzi wa kudumu wa matatizo ya afya. Je, wafikiri kwamba wakati ambapo hakuna mtu atakayekuwa mgonjwa utapata kufika? [Ruhusu itikio.] Ona taarifa hii yenye kuvutia.” Soma Isaya 33:24. Kisha fungua somo la 5 katika broshua Anataka, na uzungumzie fungu la 5-6, ukiuliza maswali yanayolingana mwanzoni mwa somo na kuchunguza maandiko machache yaliyotajwa. Taja kwamba kuondolewa kwa ugonjwa na kifo ni sehemu ya utimizo wa kusudi la Mungu la awali kwa dunia. Panga urudi kuzungumzia fungu la 1-4 na la 7 katika somo hilohilo.

4 Ikiwa habari ya sasa inayohusu kifo kisichotazamiwa imekuwa akilini mwa watu, unaweza kujaribu mfikio huu:

◼ “Huenda ukawa umesikia kuhusu [taja habari hiyo]. Maisha yafupishwapo kwa njia ya kuhuzunisha, wengi hujiuliza ni faraja gani iwezayo kutolewa familia za wahasiriwa. Wafikirije?” Ruhusu itikio. Kisha fungua ukurasa wa 299 katika kitabu Upeo wa Ufunuo, na uonyeshe mandhari ya ufufuo iliyotolewa kielezi. Endelea kwa kusema hivi: “Watu wengi hushangaa kupata kujua kwamba watu waadilifu na wasio waadilifu watarudishwa kwenye uhai katika Paradiso duniani. [Soma Matendo 24:15 kama ilivyonukuliwa katika fungu la 9 kwenye ukurasa wa 297, kisha utoe ufafanuzi unaopatikana katika fungu la 10.] Kitabu hiki huzungumzia mambo mengine mengi yenye kupendeza kuhusu kusudi la Mungu la wakati ujao. Ikiwa ungependa kujifunza mengi zaidi kulihusu, unaweza kuchukua nakala hii.” Fanya mipango ya kurudi, ukiangalia mapendezi na mahangaiko mahususi ya mtu huyo.

5 Unaporudi tena, patanisha utoaji wako na mwenye nyumba. Labda waweza kusema hivi:

◼ “Mara ya mwisho tulipoongea, nilithamini maelezo uliyotoa kuhusu kusudi la Mungu kwa dunia. [Rudia maelezo hayo.] Nilipata habari fulani ninayofikiri utapendezwa nayo.” Fungua broshua Anataka kwenye somo la 5. Soma na uzungumzie mafungu mengi iwezekanavyo katika somo hilo kadiri mwenye nyumba aonyeshavyo upendezi. Baada ya kuweka wakati wa kurudi ili kuendelea na somo hilo, mpe mwenye nyumba kikaratasi cha ukaribishaji kinachoonyesha saa za mikutano ya kutaniko, ikiwa chapatikana. Eleza juu ya Mkutano wa Watu Wote, na umwalike ahudhurie.

6 Ukipendelea utoaji uliofanywa sahili ukaziao trakti, labda waweza kusema hivi:

◼ “Ningependa kukuachia trakti hii yenye kichwa Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?” Mpe mwenye nyumba, na umwalike afuatane nawe unaposoma fungu la kwanza. Mruhusu ajibu swali lililotokezwa katika sentensi ya mwisho. Soma fungu la pili, kisha ufungue kwenye picha iliyo kwenye ukurasa wa 299 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Endelea kwa kusema: “Kitabu hiki hutoa mambo mengi zaidi kuhusu ufufuo na ahadi zile nyingine za ajabu za Biblia kwa wakati ujao. Ikiwa utakisoma, unaweza kubaki na nakala hii kwa mchango mdogo wa——.” Panga kufanya ziara ya kurudia.

7 Kutoa kwetu mwaliko wenye kuvutia kwa wengine huenda kukawafanya waje kwenye maji ya uhai, ambayo Yehova sasa anayafanya yapatikane. Kwa hiyo, acheni tumwambie kila mtu aliye na kiu, “Njoo!”—Ufu. 22:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki