Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • re sura 41 kur. 295-300
  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
  • Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Siku ya Hukumu ya Miaka Elfu
  • Nani Wanainuliwa na Kuhukumiwa?
  • Hati-Kunjo ya Uhai
  • Kufungua Hati-Kunjo Nyingine
  • Mwisho wa Kifo na Hadesi
  • Siku ya Hukumu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ule Ufalme na lile Tumaini la Ufufuo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Tumaini la Ufufuo Linamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Je, Jina Lako Liko Katika “Kitabu cha Uzima”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
re sura 41 kur. 295-300

Sura ya 41

Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!

Njozi ya 15—Ufunuo 20:11–21:8

Habari: Ufufuo wa watu wote, Siku ya Hukumu, na baraka za mbingu mpya na dunia mpya

Wakati wa utimizo: Utawala wa Miaka Elfu

1. (a) Aina ya binadamu ilipoteza nini wakati Adamu na Hawa walipofanya dhambi? (b) Ni kusudi gani la Mungu ambalo halijabadilika, na twajuaje?

TUKIWA wanadamu, tuliumbwa tuishi milele. Kama Adamu na Hawa wangalitii amri za Mungu, hawangalikufa. (Mwanzo 1:28; 2:8, 16, 17; Mhubiri 3:10, 11) Lakini walipofanya dhambi, walipoteza ukamilifu na uhai kwa ajili yao wenyewe na pia kwa ajili ya wazao wao, na kifo kikaja kutawala juu ya aina ya binadamu kikiwa adui asiyehurumia. (Warumi 5:12, 14; 1 Wakorintho 15:26) Hata hivyo, kusudi la Mungu la kuwa na wanadamu wakamilifu wakiishi milele juu ya dunia paradiso halikubadilika. Kwa sababu ya upendo wake mwingi kwa aina ya binadamu, yeye alituma duniani Mwana wake mzaliwa pekee, Yesu, ambaye alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu uwe ukombozi kwa ajili ya “wengi” wa wazao wa Adamu. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Sasa Yesu anaweza kutumia huu ubora wa kisheria wa dhabihu yake ili kurudisha wanadamu wenye kuitikadi kwenye ukamilifu wa uhai katika dunia paradiso. (1 Petro 3:18; 1 Yohana 2:2) Aina ya binadamu ina sababu tukufu kama nini ya ‘kujawa na shangwe na kushangilia’!—Isaya 25:8, 9, NW.

2. Yohana anaripoti nini kwenye Ufunuo 20:11, na “kiti cha ufalme kikubwa cheupe” ni nini?

2 Shetani akiwa amefungiwa ndani ya abiso, Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu unaanza. Sasa ni “siku” ambayo katika hiyo Mungu “anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa kwa uadilifu kwa mtu mmoja ambaye yeye ameweka rasmi.” (Matendo 17:31, NW; 2 Petro 3:8) Yohana ajulisha wazi: “Na mimi nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na mmoja aliyeketi juu yacho. Kutoka mbele zake dunia na mbingu zikakimbilia mbali, na mahali hapakupatikana kwa ajili yazo.” (Ufunuo 20:11, NW) Hiki “kiti cha ufalme kikubwa cheupe” ni nini? Hakiwezi kuwa kingine kuliko kikalio cha hukumu cha “Mungu Hakimu wa wote.” (Waebrania 12:23, NW) Sasa yeye atahukumu aina ya binadamu kwa habari ya ni nani atanufaika na dhabihu ya ukombozi ya Yesu.—Marko 10:45.

3. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba kiti cha ufalme cha Mungu kinasemwa kuwa “kikubwa” na “cheupe”? (b) Ni nani watakuwa wakihukumu kwenye Siku ya Hukumu, na kwa msingi gani?

3 Kiti cha ufalme cha Mungu ni “kikubwa,” kikikazia ukuu wa Yehova akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, na ni “cheupe,” kuvuta uangalifu kwenye uadilifu wake usio na kasoro. Yeye ndiye Hakimu wa mwisho kabisa wa aina ya binadamu. (Zaburi 19:7-11; Isaya 33:22; 51:5, 8) Hata hivyo, yeye amempa Yesu Kristo wakala wa kufanya kazi ya kuhukumu: “Baba hahukumu yeyote kabisa, bali yeye ameaminisha Mwana kuhukumu kote.” (Yohana 5:22, NW) Pamoja na Yesu ni washirika wake 144,000, ambao “nguvu za kuhukumu zilipewa kwao . . . kwa miaka elfu moja.” (Ufunuo 20:4, NW) Hata hivyo, viwango vya Yehova ndivyo vinaamua kitakachompata kila mtu mmoja mmoja wakati wa Siku ya Hukumu.

4. Maana yake nini kwamba “dunia na mbingu zikakimbilia mbali”?

4 Ni jinsi gani “dunia na mbingu zikakimbilia mbali”? Hii ni mbingu ile ile ambayo iliondoka kama hati-kunjo wakati wa kufunguliwa kifungo cha sita—serikali za kibinadamu zenye kutawala ambazo “zimewekwa akiba kwa ajili ya moto na zinawekwa kwa ajili ya siku ya hukumu na ya kuharibiwa kwa watu wasiohofu Mungu.” (Ufunuo 6:14; 2 Petro 3:7, NW) Dunia ni mfumo wa mambo uliopangwa kitengenezo ulio chini ya utawala huu. (Ufunuo 8:7) Uharibifu wa hayawani-mwitu na wafalme wa dunia na majeshi yao, pamoja na wale waliopokea alama ya hayawani-mwitu na wale waliotoa ibada kwa mfano wake, hutia alama ya kukimbilia mbali kwa hii mbingu na dunia. (Ufunuo 19:19-21) Hukumu ikiwa imetekelezwa juu ya dunia na mbingu za Shetani, Hakimu Mkuu aamuru kuwe na Siku ya Hukumu nyingine.

Siku ya Hukumu ya Miaka Elfu

5. Baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali, ni nani wanaobaki kuhukumiwa?

5 Ni nani wanaobaki wahukumiwe baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali? Si mabaki wapakwa-mafuta wa 144,000, kwa maana hawa wamekwisha hukumiwa na kutiwa muhuri. Ikiwa wapakwa-mafuta wowote bado watakuwa duniani baada ya Har–Magedoni, lazima wafe muda mfupi baada ya hapo na kupokea thawabu yao ya kimbingu kwa ufufuo. (1 Petro 4:17; Ufunuo 7:2-4) Hata hivyo, mamilioni ya umati mkubwa ambayo sasa yametoka katika dhiki kubwa yanasimama kwa wazi “mbele ya kiti cha ufalme.” Hawa wamekwisha kuhesabiwa kuwa waadilifu kwa ajili ya kuokolewa kwa sababu ya imani yao katika damu iliyomwagwa ya Yesu, lakini hukumu yao lazima iendelee kupitia muda wote wa miaka elfu kadiri Yesu aendeleavyo kuwaongoza kwenye “vibubujiko vya maji ya uhai.” Kisha, wakiwa wamekwisha rudishwa kwenye ukamilifu wa kibinadamu na baada ya hapo kutahiniwa, wao watajulishwa wazi kuwa waadilifu katika maana iliyo kamili zaidi sana. (Ufunuo 7:9, 10, 14, 17, NW) Watoto ambao huenda wakaokoka dhiki kubwa na watoto wowote wanaozaliwa kwa umati mkubwa wakati wa Mileani hali kadhalika watahitaji kuhukumiwa wakati wa miaka elfu.—Linga Mwanzo 1:28; 9:7; 1 Wakorintho 7:14.

6. (a) Ni msongamano gani anaoona Yohana, na ni nini linaloonyeshwa na maneno “wakubwa na wadogo”? (b) Mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu pasipo shaka yatatokezwaje?

6 Hata hivyo, Yohana aona msongamano mwingine wenye hesabu kubwa zaidi sana kuliko umati mkubwa wenye kuokoka. Utakuwa na hesabu yenye kufika maelfu ya mamiloni! “Na mimi nikaona wafu, wakubwa na wadogo, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na hati-kunjo zilifunguliwa.” (Ufunuo 20:12a, NW) “Wakubwa na wadogo” hutia ndani walio mashuhuri pamoja na wasio mashuhuri sana wa wanadamu ambao wameishi na wakafa kwenye dunia hii wakati wa miaka 6,000 iliyopita. Katika Gospeli ambayo Yohana aliandika muda mfupi baada ya Ufunuo, Yesu alisema kwa habari ya Baba yake: “Naye akampa [Yesu] amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:27-29) Ni mradi mkubwa ajabu kama nini—kutangua vifo na makaburi ya muda wote wa historia! Hapana shaka hayo mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu watatokezwa hatua kwa hatua hivi kwamba umati mkubwa—ambao ni wachache sana kwa kulinganisha—utaweza kushughulikia matatizo ambayo huenda yatazuka kwa sababu huenda mwanzoni wafufuliwa wakaelekea kufuata mtindo wao wa maisha ya kale, pamoja na udhaifu wa mnofu wao na mielekeo.

Nani Wanainuliwa na Kuhukumiwa?

7, 8. (a) Ni hati-kunjo gani inayofunguliwa, na ni jambo gani linalotukia baada ya hapo? (b) Ni kwa akina nani hakutakuwa na ufufuo?

7 Yohana anaongeza: “Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na wafu walihukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao. Na bahari ikatoa wafu wale walio ndani yayo na kifo na Hadesi vikatoa wafu wale walio ndani yavyo na wao walihukumiwa mmoja mmoja kulingana na matendo yao.” (Ufunuo 20:12b, 13, NW) Tamasha yenye kusisimua kweli kweli! ‘Bahari, kifo, na Hadesi’ kila mojapo inatimiza sehemu, lakini angalia kwamba semi hizi si za pekee baina yazo zenyewe.a Wakati Yona alipokuwa tumboni mwa samaki mmoja na kwa hiyo akawa katikati ya bahari, yeye alisema juu yake mwenyewe kuwa alikuwa katika Sheoli, au Hadesi. (Yona 2:2) Ikiwa mtu anashikwa na kifo cha Adamu, basi yaelekea yeye pia yumo katika Hadesi. Maneno haya ya kiunabii yanatoa uhakikisho imara kwamba hakuna hata mmoja atakayekosa kuonwa.

8 Bila shaka, kuna hesabu isiyojulikana ambayo haitafufuliwa. Miongoni mwa hawa wangekuwa waandishi na Mafarisayo waliomkataa Yesu na mitume, “mtu wa uasi-sheria” wa kidini, na Wakristo wapakwa-mafuta “ambao wameangukia mbali.” (2 Wathesalonike 2:3; Waebrania 6:4-6; Mathayo 23:29-33, NW) Yesu alisema pia juu ya watu walio kama mbuzi wakati wa mwisho wa huu ulimwengu ambao huenda ndani ya “moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake,” yaani, “kukatiliwa mbali milele.” (Mathayo 25:41, 46, NW) Hakuna ufufuo kwa hao!

9. Mtume Paulo anaonyeshaje kwamba baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo, na hao wanatia ndani akina nani?

9 Kwa upande mwingine, baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo huu. Mtume Paulo alionyesha hivyo wakati aliposema: “Mimi nina tumaini kuelekea Mungu . . . kwamba kutakuja kuwa na ufufuo wa wote walio waadilifu na wasio waadilifu.” (Matendo 24:15, NW) Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, “walio waadilifu” watatia ndani wanaume na wanawake waaminifu wa kale—Abrahamu, Rahabu, na wengine wengi—ambao walijulishwa wazi kuwa waadilifu kwa habari ya kuwa na urafiki na Mungu. (Yakobo 2:21, 23, 25) Katika kikundi iki hiki watakuwamo wale kondoo wengine waadilifu ambao walikufa wakiwa waaminifu kwa Yehova katika nyakati za ki-siku-hizi. Yaelekea, washika ukamilifu wote hao watafufuliwa mapema katika Utawala wa Mileani wa Yesu. (Ayubu 14:13-15; 27:5; Danieli 12:13; Waebrania 11:35, 39, 40) Pasi na shaka wengi wa hawa waadilifu waliofufuliwa watapewa migawo ya pendeleo la pekee katika kusimamia kazi kubwa mno ya urudisho katika Paradiso.—Zaburi 45:16; linga Isaya 32:1, 16-18; 61:5; 65:21-23.

10. Kati ya wale watakaofufuliwa, ni nani “wasio waadilifu”?

10 Ingawa hivyo, ni nani “wasio waadilifu” wanaotajwa katika Matendo 24:15, NW? Hawa wangetia ndani matungamo ya aina ya binadamu ambayo yamekufa muda wote wa historia, hasa wale ambao waliishi katika ‘nyakati za ujinga.’ (Matendo 17:30) Hawa, kwa sababu ya mahali walipozaliwa au wakati walimoishi, hawakuwa na fursa ya kujifunza kutii penzi la Yehova. Kwa kuongezea, huenda kukawa na baadhi ya waliosikia ujumbe wa wokovu lakini ambao hawakuitikia kikamili katika wakati huo au ambao walikufa kabla ya wao kuendelea kufikia wakfu na ubatizo. Katika ufufuo watu kama hao watahitaji kufanya marekebisho zaidi katika kufikiri na mwendo wao wa maisha ikiwa wao watanufaika na fursa hii kwa ajili ya kupata uhai wa milele.

Hati-Kunjo ya Uhai

11. (a) “Hati-kunjo ya uhai” ni nini, na ni majina ya nani yaliyorekodiwa katika hati-kunjo hii? (b) Ni kwa nini hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu?

11 Yohana husema juu ya “hati-kunjo ya uhai.” Hayo ni maandishi ya wale walio katika mstari wa kupokea uhai wa milele kutoka kwa Yehova. Majina ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu, ya umati mkubwa, na ya watu waaminifu wa kale, kama vile Musa, yameandikwa katika hati-kunjo hii. (Kutoka 32:32, 33; Danieli 12:1; Ufunuo 3:5, NW) Bado kufikia hapa, hakuna hata mmoja wa wale “wasio waadilifu” waliofufuliwa aliye na jina lake limeandikwa katika hati-kunjo ya uhai. Kwa hiyo hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu kuruhusu kuandikwa kwa majina ya wengine ambao wanakuja kustahili. Wale ambao majina yao hayapati kuandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai ‘wanavurumishwa ndani ya ziwa la moto.’—Ufunuo 20:15, NW; linga Waebrania 3:19.

12. Ni nini kitakachoamua kama mtu ataandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa, na Hakimu mwekwa wa Yehova aliwekaje kielelezo?

12 Basi, ni nini kitakachoamua kama mtu anapata kuandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa wakati huo? Sababisho kuu litakuwa lile lile kama lilivyokuwa katika siku ya Adamu na Hawa: utii kwa Yehova. Kama vile mtume Yohana alivyoandikia Wakristo wenzake wapendwa: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.” (1 Yohana 2:4-7, 17, NW) Kwa habari ya utii, Hakimu mwekwa wa Yehova aliweka kielelezo: “Ingawa [Yesu] alikuwa Mwana, yeye alijifunza kutii kutokana na vitu ambavyo yeye aliteseka; na baada ya yeye kuwa amefanywa mkamilifu, yeye alipata kuwa mwenye daraka la wokovu wa milele kwa wale wote wanaotii yeye.”—Waebrania 5:8, 9, NW.

Kufungua Hati-Kunjo Nyingine

13. Ni lazima wafufuliwa waonyesheje utii wao, na ni kanuni gani ambazo lazima wafuate?

13 Ni lazima hawa wafufuliwa waonyesheje utii wao? Yesu mwenyewe alielekeza kwenye amri mbili kubwa, akisema: “Ya kwanza ni, ‘Sikia O Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo mzima wote na kwa nafsi nzima yote na kwa akili nzima zote na kwa uthabiti mzima wote.’ Ya pili ni hii, ‘Lazima wewe upende jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Marko 12:29-31, NW) Pia kuna kanuni za Yehova zilizoimarishwa vizuri ambazo lazima wafuate, kama vile kukataa katakata kuiba, kusema uwongo, kuua kimakusudi, na utovu wa adili.—1 Timotheo 1:8-11; Ufunuo 21:8.

14. Ni hati-kunjo gani nyingine zinazofunguliwa, na ni mambo gani yaliyomo?

14 Hata hivyo, ndipo Yohana ametoka tu kutaja hati-kunjo nyingine ambazo zitafunguliwa wakati wa Utawala wa Mileani. (Ufunuo 20:12) Hizi zitakuwa nini? Nyakati fulani, Yehova ametoa maagizo yaliyo waziwazi katika hali maalumu. Mathalani, katika siku ya Musa yeye aliandaa mfululizo wa sheria zenye mambo mengi-mengi ambazo zilimaanisha uhai kwa Waisraeli ikiwa wangetii. (Kumbukumbu 4:40; 32:45-47) Wakati wa karne ya kwanza, maagizo mapya yalitolewa kusaidia waaminifu kufuata kanuni za Yehova chini ya mfumo wa mambo wa Kikristo. (Mathayo 28:19, 20; Yohana 13:34; 15:9, 10) Sasa Yohana anaripoti kwamba wafu ‘watahukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao.’ Kwa wazi, basi, kufunguliwa kwa hati-kunjo hizi kutatangaza matakwa ya Yehova yenye mambo mengi-mengi kwa ajili ya aina ya binadamu wakati wa miaka elfu. Kwa kutumia katika maisha yao virekebi na amri za hati-kunjo hizo, wanadamu watiifu wataweza kurefusha siku zao, wakifikia mwishowe uhai wa milele.

15. Ni kampeni ya kielimu ya aina gani itakayohitajiwa wakati wa ufufuo, na yaelekea ufufuo utaendeleaje?

15 Ni kampeni iliyopanuka kama nini ya elimu ya kitheokrasi itakayohitajiwa! Katika 2005 Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote walikuwa wakiongoza, kwa wastani, mafunzo ya Biblia 6,061,534 katika mahali pa namna namna. Lakini wakati wa ufufuo, mamilioni yasiyohesabika ya mafunzo, msingi wayo ukiwa Biblia na hati-kunjo mpya, yataongozwa bila shaka! Watu wote wa Mungu watahitaji kuwa walimu na kujitahidi wenyewe. Wafufuliwa, kadiri waendeleavyo, pasipo shaka watashiriki programu hii iliyo kubwa mno ya kufundisha. Yaelekea, ufufuo utaendelea katika njia ya kwamba wale walio hai watapata kuwa na shangwe ya kukaribisha na kufundisha washiriki wa jamaa wa zamani na watu waliojuana nao, ambao, nao kwa zamu yao, watapata kukaribisha na kufundisha wengine. (Linga 1 Wakorintho 15:19-28, 58.) Wale Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni sita ambao ni watendaji katika kueneza ukweli leo wanaweka msingi mwema kwa ajili ya mapendeleo wanayotumainia kupata katika wakati wa ufufuo.—Isaya 50:4; 54:13.

16. (a) Ni majina ya nani ambayo hayataandikwa katika hati-kunjo, au kitabu, ya uhai? (b) Ni nani wale ambao ufufuo wao utathibitika kuwa “wa uhai”?

16 Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, Yesu alisema kwamba ‘wale waliofanya mema hutoka na kuja kwenye ufufuo wa uhai, wale waliozoea vitu vibaya sana kwenye ufufuo wa hukumu.’ Hapa “uhai” na “hukumu” hutofautiana, kuonyesha kwamba wale wafufuliwa ambao ‘huzoea vitu vibaya sana’ baada ya kufundishwa katika Maandiko na hati-kunjo zilizovuviwa huhukumiwa kuwa hawastahili uhai. Majina yao hayataandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai. (Yohana 5:29, NW) Inaweza kuwa hivyo pia kwa wowote ambao hapo kwanza walifuata mwendo wa uaminifu lakini ambao, kwa sababu fulani, wanakengeuka katika wakati wa Utawala wa Miaka Elfu. Majina yanaweza kufutwa. (Kutoka 32:32, 33) Kwa upande mwingine, wale ambao kwa kutii hufuata vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo watatunza majina yao katika rekodi iliyoandikwa, hati-kunjo ya uhai, na kuendelea kuishi. Kwa wao, ufufuo utakuwa umethibitika kuwa “wa uhai.”

Mwisho wa Kifo na Hadesi

17. (a) Ni tendo gani zuri ajabu ambalo Yohana anaeleza? (b) Hadesi inaachwa tupu lini? (c) Kifo cha Adamu ‘kitavurumishwa ndani ya ziwa la moto lini’?

17 Kisha, Yohana anaeleza jambo fulani ambalo kweli ni zuri ajabu! “Na kifo na Hadesi vilivurumishwa ndani ya ziwa la moto. Hii humaanisha kifo cha pili, ziwa la moto. Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kitabu cha uhai alivurumishwa ndani ya ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14, 15, NW) Kufikia mwisho wa Siku ya Hukumu ya mileani, “kifo na Hadesi” vinaondolewa kabisa. Ni kwa nini hili lahusisha miaka elfu moja? Hadesi, ambalo ni kaburi la ujumla la aina ya binadamu, inaachwa ikiwa tupu wakati mtu wa mwisho aliye katika kumbukumbu la Mungu anapofufuliwa. Lakini maadamu binadamu wowote wanatiwa waa na dhambi iliyorithiwa, kifo cha Adamu kingali kipo pamoja nao. Wale wote wanaofufuliwa duniani, pamoja na umati mkubwa unaookoka Har–Magedoni, watahitaji kutii yaliyoandikwa katika hati-kunjo mpaka ubora wa dhabihu ya Yesu uwe umetumiwa kikamili ukiondoa magonjwa, uzee, na udhaifu mwingine uliorithiwa. Ndipo kifo cha Adamu, pamoja na Hadesi, ‘vinapovurumishwa ndani ya ziwa la moto.’ Vitakuwa vimeenda milele!

18. (a) Mtume Paulo anaelezaje habari ya fanikio la utawala wa Yesu akiwa Mfalme? (b) Yesu hufanya nini na jamaa ya kibinadamu kamilifu? (c) Kunatukia vitu gani vingine mwishoni mwa miaka elfu?

18 Hivyo, programu ambayo mtume Paulo anaeleza katika barua yake kwa Wakorintho itafikia ukamilisho: “Kwa maana lazima [Yesu] atawale akiwa mfalme mpaka Mungu ameweka maadui wote chini ya nyayo zake. Akiwa ndiye adui wa mwisho, kifo [cha Adamu] kitaletwa kwenye si kitu.” Kwafuata nini? “Wakati vitu vyote vitakuwa vimetiishwa kwake, ndipo Mwana mwenyewe pia atajitiisha mwenyewe kwa Mmoja ambaye alitiisha vitu vyote kwake.” Kwa maneno mengine, Yesu ‘amkabidhi ufalme Mungu na Baba yake.’ (1 Wakorintho 15:24-28, NW) Ndiyo, Yesu, akiwa amekwisha shinda kifo cha Adamu kupitia ubora wa dhabihu ya ukombozi wake, atakabidhi Baba yake, Yehova, jamaa ya kibinadamu kamilifu. Kwa wazi ni hapa mwishoni mwa miaka elfu, ndipo Shetani anaachiliwa na mtihani wa mwisho kabisa unafanyika kuamua ni majina ya nani yatabaki daima yamerekodiwa katika hati-kunjo ya uhai. “Jitahidini wenyewe kisulubu” ili jina lenu liwe miongoni mwayo!—Luka 13:24; Ufunuo 20:5, NW.

[Maelezo ya Chini]

a Wale wanaofufuliwa kutoka katika bahari hawangetia ndani wakazi wafisadi wa dunia walioangamia katika Gharika ya siku ya Noa; uharibifu huo ulikuwa wa kukata maneno, kama utakavyokuwa utekelezo wa hukumu ya Yehova katika dhiki kubwa.—Mathayo 25:41, 46; 2 Petro 3:5-7.

[Picha katika ukurasa wa 298]

Wafufuliwa “wasio waadilifu” ambao hutii hati-kunjo zinazofunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu huenda wakaandikisha pia majina yao katika ile hati-kunjo ya uhai

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki