Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Februari: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! kwa bei ya pekee iliyoruhusiwa katika nchi yenu. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kazia kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani. Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaopata ugumu wa kutimiza takwa la saa, wazee wapaswa kupanga ili usaidizi utolewe. Ili kupata madokezo, pitia barua ya Sosaiti (S-201-SW) ya Oktoba 1, 1993, na Oktoba 1, 1992. Pia ona fungu la 12-20 la nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
◼ Wahubiri ambao wamefanya mipango ya kushiriki kuhubiri eneo lisilogawiwa mtu miezi ya wakati ujao vyapaswa kupanga kutoa broshua Anataka au kitabu Ujuzi katika utumishi wao wa shambani.
◼ Baraza la wazee lapaswa kujua kwamba marekebisho yafuatayo yanahitajiwa wakati kutaniko linapohudhuria makusanyiko ya kwalo: Wakati ambapo programu ya siku ya kusanyiko la pekee imeratibiwa, kutaniko lapaswa kuwa na mikutano yote ya kawaida muda wote wa juma hilo, isipokuwa kwamba Mkutano wa Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi hufutwa. Linaporatibiwa kuhudhuria kusanyiko la mzunguko, kutaniko litafuta pia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi; ila Funzo la Kitabu la Kutaniko litafanywa mahali hapo juma hilo.
◼ Vichapo Vinavyopatikana:
Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa —Kichina (Sahili), Kitigrinya
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? —Kitigrinya
Your Will Be Done on Earth —Kiingereza
◼ Vidiokaseti Mpya Zinazopatikana:
Jehovah’s Witnesses Stand Firm Against Nazi Assault —Kifaransa