Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/98 uku. 8
  • Kutolea Ushahidi “Watu wa Namna Zote”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutolea Ushahidi “Watu wa Namna Zote”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Utangulizi wa Kitabu Mankind’s Search for God
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 6/98 uku. 8

Kutolea Ushahidi “Watu wa Namna Zote”

1 Tunapokutana na watu wa tamaduni au dini mbalimbali, twakumbuka kwamba mapenzi ya Yehova ni “kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Kuongezea trakti kadhaa na broshua zilizotayarishwa kipekee, tuna vichapo viwili vilivyo bora kabisa viwezavyo kutumiwa wakati wowote kusaidia watu ambao dini zao hazijawafundisha kweli kuhusu Mungu na Kristo.

2 Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu hutoa ufahamu wenye kina katika chanzo cha dini kuu za ulimwengu na hivyo chaweza kuwa chenye msaada kwa watu kila mahali katika kulinganisha itikadi zao na yale ambayo Biblia hufunza kuhusu Mungu wa pekee wa kweli. Kwa upande mwingine, kwa kukazia maisha ya Yesu Kristo, kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi chaweza kumsaidia mtu amfahamu vizuri zaidi Mwana wa Mungu na kuvutwa kwake, kama walivyovutwa watu wengi katika karne ya kwanza. (Yn. 12:32) Mahali popote pafaapo, huenda ukataka kujaribu madokezo yafuatayo ya kutoa vitabu hivi ambavyo tutatoa kwa bei za pekee kama ilivyotangazwa awali.

3 Ukiona itafaa kumtolea mtu kitabu “Mtu Mkuu,” unaweza kuuliza:

◼ “Ufikiripo juu ya Yesu Kristo ni mawazo gani huja akilini mwako? [Mruhusu ajibu.] Wanahistoria wengi humkiri Yesu kuwa yule mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi. [Nukuu kielelezo kutoka katika utangulizi ulio katika kitabu Mtu Mkuu.] Biblia huonyesha kwamba maisha ya Yesu yalikuwa kigezo kwetu ili tumwige.” Soma 1 Petro 2:21 na fungu la kwanza kwenye ukurasa wa mwisho wa utangulizi wa kitabu Mtu Mkuu. Mwenye nyumba akipendezwa kujifunza juu ya Yesu, mtolee kitabu. Kabla hujaondoka, soma Yohana 17:3 na uulize, “Twaweza kutwaaje ujuzi huu uongozao kwenye uhai udumuo milele?” Fanya mipango hususa ya kurudi ukiwa na jibu.

4 Unaporudi kueleza jinsi ya kutwaa ujuzi wenye kuokoa uhai, waweza kusema hivi:

◼ “Niliahidi kurudi ili nikuonyeshe jinsi tunavyoweza kutwaa ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele.” Toa kitabu Ujuzi, na ukitumia sura ya kwanza, uonyeshe jinsi ya kujifunza.

5 Ukitaka kutoa kitabu “Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu,” waweza kuuliza hivi:

◼ “Kukiwa na dini nyingi sana leo zilizo tofauti, je, umepata kujiuliza jinsi tunavyoweza kuamua ni ipi inayokubaliwa na Mungu?” Akishajibu, fungua kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kwenye ukurasa wa 377. Kazia hoja namba 7, na uulize kama mwenye nyumba akubali kwamba dini ya kweli yapaswa kuunganisha jamii zote za wanadamu. Someni andiko moja lililotajwa, na kadiri wakati uruhusuvyo, zungumzieni baadhi ya hoja zilizoorodheshwa kisha, utoe kitabu. Unapoondoka, ungeweza kuuliza, “Dini ya kweli yapasa kuwa na athari gani kwa mwenendo wa mtu?” Panga kufanya ziara ya kurudia na kujibu swali hilo.

6 Unaporudi kueleza jinsi ambavyo dini ya kweli huathiri maisha ya mtu, waweza kuuliza hivi:

◼ “Wafikiri dini yapaswa kuathirije mwenendo wa watu? [Mruhusu ajibu.] Kristo alitupa kiwango ambacho twaweza kukadiria dini.” Soma Mathayo 7:17-20 moja kwa moja kutoka kwenye ukurasa wa 12 katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Kisha mwalike mwenye nyumba asome fungu la 20 kwenye ukurasa wa 12-13. Wakati ukiruhusu, zungumzia fungu la 25-29 kwenye ukurasa wa 15-18. Hilo laweza kuongoza kwenye funzo ama katika broshua Anataka ama kitabu Ujuzi.

7 Vianzisha-Mazungumzo: Kuna misaada mingi ya kufundisha katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ambayo yaweza kutumiwa kuwa vianzisha-mazungumzo katika ziara ya kwanza au kwenye ziara ya kurudia. Waweza kuanzisha mazungumzo kwa kuuliza tu swali lifaalo. Kwa mfano, ona maswali na habari hizi za mazungumzo na mahali zinapopatikana:

“Maswali Yanayotaka Jibu”—ukurasa wa 17-18.

“Je! Yesu Alikuwa Ngano Tu?”—ukurasa wa 237.

“Nani Aliandika Biblia?”—ukurasa wa 241.

“Qurani na Biblia”—ukurasa wa 285.

“Uthibitisho wa Uasilia wa Biblia”—ukurasa wa 340-341.

“Wanayoamini Mashahidi wa Yehova”—ukurasa wa 356-357.

“Jinsi ya Kutambua Dini ya Kweli”—ukurasa wa 377.

8 Waweza kufungua ukurasa au kurasa zilizoteuliwa katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu nawe ueleze hoja inayozungumziwa. Kisha panga ziara ya kurudia kwa kuuliza swali linalohusiana na hayo mazungumzo linaloweza kujibiwa ama kutoka broshua Anataka ama kitabu Ujuzi. Hakikisha unamwalika mwenye nyumba kwenye Mkutano wa Watu Wote na umwachie kikaratasi cha ukaribishaji ikiwa chatumika mahali hapo.

9 Watu wa namna zote wenye moyo wa haki wanatafuta kweli kuhusu Mungu na Kristo. Twaweza kuwasaidia katika kazi yetu ya kutoa ushahidi. Kwa hiyo, basi, acheni tuendelee “[ku]fanya kazi kwa bidii na kujikakamua wenyewe, kwa sababu tumeweka tumaini letu juu ya Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa namna zote za watu.”—1 Tim. 4:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki