Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/98 uku. 8
  • Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi-Msimamizi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi-Msimamizi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Mwatilie Maanani Wale Wanaofanya Kazi kwa Bidii Kati Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wazee wa Kundi—‘Simamieni Vizuri’!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 8/98 uku. 8

Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi-Msimamizi

1 Kutumikia ukiwa mwangalizi katika kutaniko ni daraka zito. (Mdo. 20:28; 1 Tim. 3:1) Hii ni makala ya kwanza ya mfululizo utakaoonyesha wajibu mbalimbali wa wazee Wakristo ili sisi sote tuweze kuthamini kazi ya maana wanayofanya kwa niaba yetu.

2 Sosaiti humweka rasmi mwangalizi-msimamizi atumikie kwa kipindi cha wakati usiojulikana. Mwangalizi-msimamizi anaposimamia mambo, hilo husaidia wazee waukazie uangalifu ufaao wajibu wao waliogawiwa. (Huduma Yetu, uku. 42) Hilo hutaka nini?

3 Mwangalizi-msimamizi hupokea barua za kutaniko na kuzipitisha upesi kwa mwandishi ili azishughulikie. Katika kutayarisha mikutano ya wazee, mwangalizi-msimamizi hupata madokezo kutoka kwa wazee kuhusu mambo yanayohitaji kuzungumziwa na kutayarisha ajenda. Yeye pia huwa mwenyekiti katika mikutano ya wazee. Maamuzi yafanywapo, yeye huhakikisha kwamba yanatimizwa ifaavyo. Yeye husimamia utayarishaji wa Mkutano wa Utumishi na kuratibu hotuba za watu wote. Yeye hutoa kibali cha matangazo yote yanayotolewa kutaniko, huidhinisha malipo ya gharama zote za kuendesha shughuli za kawaida, naye huhakikisha kwamba ukaguzi wa baada ya kila miezi mitatu wa hesabu ya kutaniko unafanywa.

4 Akiwa mwenyekiti, mwangalizi-msimamizi husimamia kazi ya Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Mwanafunzi wa Biblia aombapo kutambuliwa kuwa mhubiri asiyebatizwa au, mhubiri asiyebatizwa atakapo kubatizwa, mwangalizi-msimamizi hupanga ili wazee wengine wakutane naye. Pia mwangalizi-msimamizi huongoza katika kutayarisha ziara ya mwangalizi wa mzunguko ili kutaniko linufaike kikamili na juma la utendaji wa pekee.

5 Wajibu wa mwangalizi-msimamizi ni mwingi na ni wa aina mbalimbali. Atunzapo madaraka yake kwa unyenyekevu akiwa na “bidii halisi,” sisi sote twaweza kufanya sehemu yetu kwa kushirikiana na wazee. (Rom. 12:8) Tukiwa “watiifu” na “wenye kunyenyekea” wale wanaoongoza miongoni mwetu, wanaweza kufanya kazi yao wakiwa na shangwe ya kweli nyingi zaidi.—Ebr. 13:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki