Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/98 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 8/98 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la fasihi la Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 zaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?, na Serikali Itakayoleta Paradiso. Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa popote panapozifaa. Kuongezea, tutakuwa na toleo la pekee la vijitabu Roho Zisizoonekana—Je! Zinatusaidia? au Zinatuumiza? na Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona kama ilivyoonyeshwa katika barua kutoka ofisi ya tawi. Wahubiri na mapainia wote wanatiwa moyo kutumia vijitabu hivi kwa wingi wakati wa kampeni ya eneo lililo peke yake. Makutaniko ambayo hayana vijitabu hivi akibani yanaweza kuviagiza sasa ili kuhakikisha akina ndugu wanavipata kwa ajili ya miezi hiyo. Septemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Oktoba: Toa andikisho la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa nakala moja-moja za magazeti hayo. Novemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.

◼ Mwaweza kujipatia mabuku yaliyojalidiwa ya kuanzia 1994 na mapema zaidi ya hapo kwa bei iliyopunguzwa chini ya nusu ya bei ya kawaida.

◼ Mwandishi wa kutaniko atakusanya ripoti za utumishi ili kuziingiza katika fomu ya Ripoti ya Mchanganuo ya Kutaniko (S-10-SW). Pia ataagiza kwa uangalifu mzee yeyote au mtumishi wa huduma ambaye huenda akawa anasaidia kuikusanya ripoti hiyo. Kufanya hivi kutahakikisha hesabu sahihi ya habari inayohitajiwa. Fomu ya Ripoti ya Mchanganuo ya Kutaniko (S-10-SW) yapasa kujazwa kwa usahihi na kwa unadhifu na ichunguzwe kwa uangalifu na halmashauri ya utumishi. Tafadhali pelekeeni Sosaiti ile ya awali kabla ya Septemba 6.

◼ Ugavi wa kutosha wa fomu za kutumia wakati wa mwaka wa utumishi wa 1999 unapelekewa kila kutaniko. Tafadhali tumieni fomu hizi kwa busara. Zapasa zitumiwe tu kama zilivyokusudiwa.

◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza 1999 Calendar of Jehovah’s Witnesses pamoja na ombi lao la fasihi la Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kiingereza na Kifaransa.

◼ Kuanzia Agosti 26, 1998, hadi Agosti 28, 1998, Sosaiti itakuwa ikihesabu fasihi zote zilizomo katika ofisi ya tawi na depo mbalimbali. Kwa sababu ya kuhesabu huku, hakuna maagizo yoyote ya fasihi ya kutaniko yatakayofanyiwa upakizi au yatakayochukuliwa siku hizo.

◼ Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko yapaswa kutoa uangalifu bila kukawia kwa maombi yote ya utumishi wa painia wa kawaida. Halmashauri ya utumishi haipaswi kuweka ombi ili kuona kama yule anayejaza anaweza kutimiza takwa la saa. Tarehe ya kuwekwa kuwa painia yaweza kubadilishwa kwenye maombi yaliyopokewa baada ya tarehe ya kujaza ombi. Ombi likichelewa, mwombaji hatawekwa kuwa painia tarehe ambayo ombi hilo lilijazwa isipokuwa kuwe na hali za pekee sana. Hali hizo ziwapo, barua yapaswa kuandamana na ombi.—Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986 fungu la 24-26.

◼ Mfululizo wa broshua utachunguzwa katika Funzo la Kitabu la Kutaniko baada ya kumaliza kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Tangazo lililotolewa katika toleo la Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1998 lilisema kwamba kuanzia juma la Septemba 21, broshua Anataka itatumiwa. Hiyo itafuatiwa na broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? na Je! Kweli Mungu Anatujali?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki