Habari Za Kitheokrasi
Kenya: Kulikuwa na kilele kikuu kupita vyote cha mapainia-wasaidizi 2,091 katika Aprili 1998. Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kufikia kiwango cha mapainia-wasaidizi 2,000 katika mwezi mmoja.
Rwanda: Majumba ya Ufalme mawili zaidi katika nchi hii yaliwekwa wakfu hivi majuzi. Hayo yalikuwa katika Kigali Gatsata na Gatumba.
Sudan: Walikuwa na hudhurio zuri la Ukumbusho ambalo lilikuwa zaidi ya mara tano ya idadi ya wahubiri!
Tanzania: Kilele cha wahubiri 7,204 katika Aprili kilifikiwa na kilele kipya cha mapainia-wasaidizi 824 kikafikiwa katika Aprili 1998.
Uganda: Mwezi wa Aprili 1998, magazeti 12,765 yaliangushwa. Hiki kilikuwa kilele kikuu kuliko vyote cha magazeti yaliyoangushwa kwa mwezi mmoja nchini humo.