Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Septemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Oktoba: Toa andikisho la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa nakala moja-moja za magazeti hayo. Novemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeagizwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyotolewa kwenye ukurasa wa 21-23 katika Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1991, kuhusu watu wowote waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wakawa na mwelekeo wa kurudishwa.
◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kutuma maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haishughulikii maagizo ya fasihi ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla agizo la kila mwezi la kutaniko la fasihi halijapelekwa kwa Sosaiti ili wote wenye kupendezwa kupata fasihi za kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani vilivyo vifaa vya kuagizwa kipekee.