Habari Za Kitheokrasi
Katika Afrika Mashariki, mizunguko minne ilianzishwa Septemba 1 kama ifuatavyo: miwili katika Kenya, mmoja katika Tanzania na mmoja katika Rwanda. Sasa tuna mizunguko 16 katika Kenya, 9 katika Tanzania, 4 katika Rwanda, 2 katika Uganda na 2 katika Sudan.
Kenya: Katika Aprili Kenya iliripoti mapainia-wasaidizi 2,091 ikiwa mara ya kwanza kuripoti zaidi ya 2,000. Zaidi ya asilimia 29 ya wahubiri wote walikuwa katika namna fulani ya utendaji wa painia.
Rwanda: Mapainia-wasaidizi wawili katika kutaniko moja huko Rwanda waliangusha magazeti 224 mwezi wa Mei.
Sudan: Hudhurio zuri la Ukumbusho la zaidi ya mara tano ya idadi ya wahubiri liliripotiwa.
Tanzania: Mwezi wa Aprili, kilele kipya cha mapainia-wasaidizi 824 kiliripotiwa.
Uganda: Kwenye programu iliyomalizika hivi karibuni ya Siku ya Kusanyiko la Pekee, kulikuwa na hudhurio zuri la watu 3,191, ambalo ni asilimia 150 hivi.