Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/98 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 12/98 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la fasihi la Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichoorodheshwa katika barua ya Februari 5, 1998 na Mei 19, 1998 ambacho huenda kutaniko likawa nacho akibani kitatolewa kwa bei ya pekee. Makutaniko ambayo hayana ugavi wa vitabu hivyo yaweza kuomba wanavyohitaji kutoka katika ofisi ya tawi au ofisi ya nchi ya kwao. Februari: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mahali ambapo hakipatikani, toa kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.

◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Watchtower na Awake! ya 1998 katika ombi lao la fasihi la Desemba. Mabuku yaliyojalidiwa yatapatikana katika Kifaransa na Kiingereza. Mabuku yaliyojalidiwa ni bidhaa za kuombwa kipekee.

◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyewekwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Desemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Jambo hili lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu itakayofuata kusomwa.

◼ Ukumbusho wa mwaka wa 2000 utakuwa Jumatano, Aprili 19, baada ya jua kushuka. Taarifa hii ya mapema imetolewa ili akina ndugu waweze kukodi au kufanya maagano ya lazima kwa majumba yanayopatikana mahali ambako kuna makutaniko kadhaa yanayotumia Jumba la Ufalme na majengo mengine lazima yatafutwe. Wazee wanapaswa kuwa na mapatano pamoja na wasimamizi wa jengo wakihakikisha kwamba hakutakuwa na usumbufu kutokana na utendaji mwingine katika jengo hilo ili kwamba mwadhimisho wa Ukumbusho uweze kuendelea kwa njia ya amani na kwa utaratibu. Kwa sababu ya umaana wa tukio hili, baraza la wazee linapompa mgawo msemaji wa Ukumbusho, lapaswa kuteua mmojawapo wa wazee mwenye kustahili zaidi badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Isipokuwa tu kuwe na mzee mwenye uwezo kati ya watiwa-mafuta anayeweza kutoa hotuba hiyo.

◼ Broshua yenye kichwa The Guidance of God—Our Way to Paradise inatayarishwa kutolewa hivi punde. Broshua hii imekusudiwa kuvutia Waislamu wanaoishi katika mazingira ambayo huenda wakahisi wakiwa huru kujifunza Biblia. Broshua hiyo yatayarishwa katika lugha zaidi ya 20. Matoleo ya lugha zinazohusika yatatangazwa yatapatikana ili maagizo yatolewe.

◼ Kukiwa na miisho-juma mitano kamili, mwezi wa Januari ni wakati mzuri kwa wengi kufanya upainia-msaidizi.

◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:

Kuanzia toleo la Januari-Machi 1999, Amkeni! litachapwa baada ya kila miezi mitatu katika Kitigrinya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki