Habari Za Kitheokrasi
Katika Agosti 1998 tulifikia kilele kipya kilichojumlishwa cha wahubiri 29,448 katika nchi zilizo chini ya ofisi yetu ya tawi. Hicho kilizidi mradi wetu wa wahubiri 28,500 ambao ulikuwa umewekwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1998.
Kenya: Jumba la Ufalme la Nzambani katika Kitui, Kenya, liliwekwa wakfu hivi majuzi.
Rwanda: Jumba la Ufalme la Cyangugu liliwekwa wakfu hivi majuzi. Hili ni Jumba la Ufalme la nne kuwekwa wakfu katika Rwanda tangu kampeni ya pekee ilipoanzishwa ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme.
Hudhurio la programu ya Siku ya Kusanyiko la Pekee katika Rwanda mwaka wa utumishi wa 1998 lilikuwa asilimia 187!