Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/98 kur. 3-4
  • Jenga Maisha Yako Katika Msingi wa Utumishi wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jenga Maisha Yako Katika Msingi wa Utumishi wa Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Panga Ratiba Inayofaa ya Familia
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Utumishi wa Painia—Je, Wakufaa Wewe?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Elekezea Sana Fikira Mpango wa Kibinafsi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Familia, Sifuni Mungu Mkiwa Sehemu ya Kutaniko Lake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 12/98 kur. 3-4

Jenga Maisha Yako Katika Msingi wa Utumishi wa Yehova

1 Yesu alifananisha wasikilizaji wake na aina mbili za wajenzi. Mmoja alijenga njia yake ya maisha juu ya mwamba wa utii kwa Kristo naye aliweza kuhimili dhoruba ya upinzani na dhiki. Yule mwingine alijenga juu ya mchanga wa utii wenye ubinafsi naye hakuweza kushinda msongo ulipokuja. (Mt. 7:24-27) Tukiishi katika umalizio wa mfumo huu wa mambo, tunapatwa na dhoruba nyingi za janga. Mwonekano wenye kuhuzunisha wa kutisha wa dhiki kubwa unakaribia upesi. Je, tutavumilia hadi mwisho imani yetu ikiwa kamili? (Mt. 24:3, 13, 21) Mengi yategemea jinsi tunavyojenga maisha zetu sasa. Hivyo, inafaa zaidi kujiuliza wenyewe, ‘Je, mimi najenga imara maisha yangu ya Kikristo katika utumishi wenye utii kwa Mungu?’

2 Kujenga maisha yetu katika msingi wa utumishi wa Yehova kwamaanisha nini? Kwamaanisha kumfanya Yehova awe jambo kuu maishani mwetu. Hutia ndani kukazia Ufalme kuwa hangaikio letu kuu. Huhitaji kumtii Mungu katika shughuli zetu za maisha ya kila siku. Huhitaji kujitoa kwa moyo wote katika funzo letu la Biblia la kibinafsi, la familia, na la kutaniko na katika huduma yetu ya shambani, tukitanguliza mambo hayo. (Mhu. 12:13; Mt. 6:33) Mwendo huo wa utii hutokeza msingi imara kabisa ambao hautaporomoka tukabilipo dhoruba za janga ambazo huenda zikatokea.

3 Inapendeza kuona mamilioni ya watu wakijenga ifaavyo maisha zao na matumaini yao ya wakati ujao katika utumishi wa Mungu, kama alivyofanya Yesu. (Yn. 4:34) Wao hushikilia ratiba thabiti ya utendaji wa kitheokrasi nao hufurahia baraka zake nyingi. Mama mmoja alieleza jinsi ambavyo yeye na mume wake wamelea wana wao wawili kwa mafanikio wamtumikie Yehova: “Tulijaza maisha zetu na kweli—kwenda kwenye mikusanyiko yote, kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na kuihudhuria, na kufanya utumishi wa shambani uwe sehemu ya kawaida ya maisha zetu.” Mume wake aliongezea hivi: “Kweli si sehemu ya maisha yetu, ni maisha yetu. Mambo mengine yote huitegemea.” Je, wewe pia umeweka utumishi wa Yehova kuwa jambo la kutangulizwa katika familia yako?

4 Panga Ratiba Iwezayo Kutumika ya Kila Juma: Tengenezo la Yehova hutusaidia kufuatia kawaida nzuri ya kiroho kwa kupanga mikutano mitano kwa juma. Wakristo ambao wanajenga maisha yao katika ibada ya Yehova hupanga mambo yao ya kimwili na ya familia katika njia ambayo wataweza kuhudhuria mikutano yote hii muhimu. Hawaruhusu mambo yasiyo na maana sana yaingilie kuhudhuria kwao mikutano kwa ukawaida.—Flp. 1:10; Ebr. 10:25.

5 Wakristo wakomavu hutambua kwamba kama ilivyo muhimu kupata milo ya kawaida nyakati fulani kila siku, ndivyo ilivyo muhimu kupanga ratiba hususa ya funzo la kibinafsi na la familia, kutia ndani utayarishaji wa mikutano. (Mt. 4:4) Je, ungeweza kuweka kando kipindi cha angalau dakika 15 au 20 kila siku kwa ajili ya funzo la kibinafsi? Ufunguo ni kutoacha mambo mengine yaingilie polepole wakati uliowekwa kando kwa ajili ya funzo. Lifanye liwe zoea linalofaa. Huenda hilo likahitaji uamke mapema kila asubuhi kuliko unavyoamka sasa. Washiriki 17,000 wa familia ya ulimwenguni pote wa Betheli huamka mapema asubuhi wawe na mazungumzo ya andiko la siku. Bila shaka, kuamka mapema kwahitaji uende kulala wakati unaofaa ili uanze siku inayofuata ukiwa katika hali nzuri na ukiwa umepumzika.

6 Ikiwa wewe ni kichwa cha familia, chukua hatua ya kwanza kupanga ratiba ya familia yako ya utendaji wa kitheokrasi. Familia fulani husoma Biblia, Yearbook, au kichapo kinginecho wakiwa pamoja wanapopumzika baada ya mlo wa jioni. Wazazi wengi ambao wameona watoto wakikua hadi kufikia kuwa Wakristo wenye nguvu kiroho husema kwamba jambo moja lililochangia mafanikio yao lilikuwa ile desturi ya familia ya kuweka wakati jioni moja kila juma ambapo walifurahia wakati wenye kujenga kiroho wakiwa pamoja. Baba mmoja alisema hivi: “Nahisi kwamba maendeleo ya kiroho ya watoto wetu yalichangiwa hasa na funzo letu la familia la ukawaida la Jumatano usiku, lililoanza miaka 30 iliyopita.” Watoto wake wote watatu walibatizwa wakiwa na umri mdogo, na baadaye wote watatu wakaingia kwenye huduma ya wakati wote. Kuongezea funzo la familia, utoaji wa utumishi wa shambani au sehemu za mikutano zaweza kufanyiwa mazoezi na shughuli nyingine zifaazo zaweza kufurahiwa pamoja.

7 Katika ratiba yako ya kila juma, je, ‘umenunua wakati’ kwa ajili ya kuhubiri Ufalme? (Kol. 4:5) Wengi wetu tuna shughuli nyingi sana, tukishughulikia madaraka ya familia na ya kutaniko. Ikiwa hatufanyi mipango hususa ya kushiriki katika kazi ya kuhubiri na kufundisha kila juma, itakuwa rahisi kukosa nafasi ya utendaji huu muhimu. Mwenye shamba kubwa la ng’ombe alisema hivi: “Mnamo 1944 nilitambua kwamba njia pekee ambayo ningeweza kuwa katika utumishi wa shambani ilikuwa tu kupanga siku fulani kwa ajili yake. Hadi leo, mimi huchukua siku nzima katikati ya juma kwa ajili ya utumishi.” Mzee mmoja Mkristo huona kwamba kuwa na ratiba hususa ya kutoa ushahidi humwezesha kufanya muda wa saa nyingi kuliko wastani wa nchi wa kila mwezi katika kazi ya kuhubiri. Ikiwa ana kazi yoyote ya kimwili Jumamosi, yeye huiratibu baada ya utumishi wake wa shambani wa asubuhi. Je, wewe na familia yako mwaweza kuratibu angalau siku moja kila juma kwa ajili ya utumishi wa shambani, mkifanya hiyo iwe sehemu ya njia yenu ya maisha ya kiroho?—Flp. 3:16.

8 Changanua Kawaida Yako ya Maisha: Kuna mambo ambayo hutuzuia tujenge maisha yetu katika utumishi wa Yehova. Hali zisizotazamiwa zaweza kuvuruga ratiba yetu iliyopangwa vizuri ya funzo, mikutano, na utumishi. Naye Adui yetu, Shetani, atafanya yote awezayo ‘kukatiza pito letu’ na kuzuia mipango yetu. (1 The. 2:18; Efe. 6:12, 13) Usiruhusu vizuizi hivi vikuvunje moyo, ili ushindwe. Fanya marekebisho yoyote yanayohitajiwa ili kutimiza ratiba yako iliyopangwa ya utendaji wa kitheokrasi. Azimio na uendelevu ni mambo yanayohitajika ili kutimiza yanayofaa kwa kweli.

9 Hatupaswi kuruhusu uvutano mbalimbali wa kilimwengu na athari mbaya ya mwili wetu usio mkamilifu ituletee shughuli zisizo za kiroho ambazo zingeweza kuanza kuchukua wakati wetu mwingi zaidi na uangalifu wetu. Twahitaji kujichunguza tukitumia maswali kama haya: ‘Je, maisha yangu yamekosa usawaziko au yamekengeuka, kusema kitamathali? Je, nimeanza kujenga maisha yangu katika vitu vya ulimwengu huu ambavyo vinapitilia mbali? (1 Yh. 2:15-17) Natumia wakati mwingi kadiri gani kwa mambo ya kibinafsi, safari za raha, shughuli za michezo, au tafrija nyinginezo—kutia ndani kutazama televisheni au kupitia-pitia Internet—kwa kulinganisha na wakati unaotumiwa kwa utendaji wa kiroho?’

10 Ukihisi kwamba maisha yako yamejaa utendaji mwingi usio wa maana, ni nini liwezalo kufanywa? Kama vile Paulo alivyosali kwamba ndugu zake ‘warekebishwe upya,’ au ‘wawekwa katika mlinganisho ulio sawasawa,’ kwa nini usitoe dua kwa Yehova akusaidie ukazie utumishi wake tena? (2 Kor. 13:9, 11, kielezi-chini katika New World Translation of the Holy Scriptures—With References) Kisha azimia kuishi kupatana na azimio lako na kufanya marekebisho yanayohitajiwa. (1 Kor. 9:26, 27) Yehova atakusaidia uepuke kugeuka upande wa kulia au upande wa kushoto wa utumishi mtiifu kwake.—Linganisha Isaya 30:20, 21.

11 Baki Ukiwa Mwenye Shughuli Nyingi Katika Utumishi Wenye Shangwe wa Mungu: Mamilioni ya watu hufuatia furaha wakiwa tayari kufanya lolote wakija kugundua tu kwamba mwisho ukaribiapo, vitu vya kimwili walivyotafuta kwa hamu, havikuwaletea furaha ya kudumu. Imekuwa “kujilisha upepo.” (Mhu. 2:11) Kwa upande mwingine, tunapoweka maisha yetu yakiwa yamekaziwa Yehova, ‘tukimweka mbele yetu daima,’ tunapata uradhi mwingi. (Zab. 16:8, 11) Inakuwa hivyo kwa sababu Yehova ndiye sababu hasa ya kuwapo kwetu. (Ufu. 4:11) Bila yeye, Mkusudiaji Mkuu, maisha hayana kusudi. Tunapomtumikia Yehova maisha yetu hujawa na utendaji unaofaa, wenye kusudi ambao hutunufaisha sisi na wengine vilevile kwa njia yenye kudumu, naam, kwa njia idumuyo milele.

12 Ni muhimu kutokuwa wenye kuridhika na kupoteza hisi yetu ya uharaka kuhusu mwisho unaokaribia upesi wa ulimwengu wa Shetani. Maisha yetu ya siku kwa siku yanaathiriwa na jinsi tunavyouona wakati ujao. Watu katika siku ya Noa, ambao hawakuamini kwamba kungekuwa na gharika ya tufeni pote, “hawakujali,” wakikazia maisha zao za kila siku kwenye mambo ya kibinafsi—kula, kunywa, na kuoa—mpaka furiko ‘likawafagilia mbali wote.’ (Mt. 24:37-39) Leo, wale wanaokazia maisha zao kwenye ulimwengu huu wataona matazamio yao ya wakati ujao yakibatilika katika uharibifu mkubwa zaidi ambao mwanadamu hajapata kuuona, “siku ya Yehova.”—2 Pet. 3:10-12.

13 Basi, fuliza kujenga maisha yako katika Mungu aishiye, Yehova, na kufanya mapenzi yake. Hakuna akiba unayoweza kuweka katika maisha haya, iliyo na Mtegemezaji mwenye kutumainika kama Yehova. Yeye hawezi kusema uwongo—atakuwa mwaminifu kwa ahadi zake. (Tito 1:2) Hawezi kufa—hakuna kitu chochote kilichowekwa akiba na Yehova kitakachopotea. (Hab. 1:12; 2 Tim. 1:12) Maisha ya utii na imani tunayojenga sasa ni mwanzo tu wa maisha yatakayodumu milele katika utumishi wenye shangwe wa Mungu wetu mwenye furaha!—1 Tim. 1:11; 6:19.

[Blabu katika ukurasa wa 3]

“Kweli si sehemu ya maisha yetu, ni maisha yetu. Mambo mengine yote huitegemea.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki