Panga Ratiba Inayofaa ya Familia
1 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu aliwahimiza hivi wasikilizaji wake: “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.” (Mt. 6:33) Njia inayofaa ya kupanga shughuli za familia ili mambo ya kiroho yatangulizwe, ni kuwa na ratiba iliyoandikwa. Tumieni dakika chache kupanga ratiba ya kila juma ya familia mkitumia ratiba ambayo haijajazwa, iliyo katika ukurasa wa 6 wa nyongeza hii. Mnaweza kuandika shughuli za familia yenu kwenye ratiba hiyo, au kukata visehemu vilivyo chini ya ratiba iliyo katika ukurasa wa 6 na kuvibandika kwenye ratiba ya familia yenu.
2 Ratiba iliyo hapa chini inaweza kuwasaidia kupanga ratiba yenu. Mtaona kwamba inahusisha mambo manne tu yaliyo muhimu: (1) kuhudhuria mikutano ya kutaniko, (2) huduma ya shambani ya familia, (3) funzo la familia, na (4) kuchunguza andiko la siku. Kupanga mambo hayo katika ratiba yenu kutawasaidia “kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Mapendekezo zaidi kuhusu mambo hayo manne yamo katika ukurasa wa 4-5.
3 Ratiba yenu ya familia haihitaji kuhusisha mambo hayo manne tu. Ikiwa ninyi hutayarisha mikutano fulani mkiwa pamoja, mnaweza kuandika jambo hilo katika ratiba yenu. Iwapo mnasoma sehemu fulani ya Biblia mkiwa pamoja baada ya kuchunguza andiko la siku au katika pindi nyingine, andikeni jambo hilo katika ratiba. Ikiwa ninyi huwa na tafrija fulani huenda mkaona kuwa inafaa kuandika jambo hilo katika ratiba yenu.
4 Pangeni ratiba ya familia kupatana na mahitaji na hali za kila mmoja katika familia yenu. Mara kwa mara, chunguzeni ikiwa ratiba yenu bado inafaa hali zenu, na mfanye marekebisho yoyote yanayohitajika.
[Chati katika ukurasa wa 3]
Ratiba ya Mfano ya Familia
Asubuhi Alasiri Jioni
J2. Andiko la Siku
Hotuba ya Watu Wote na
Funzo la Mnara wa Mlinzi
J3. Andiko la Siku Funzo la Familia
J4. Andiko la Siku Funzo la Kitabu
la Kutaniko
J5. Andiko la Siku
Al. Andiko la Siku Shule ya Huduma
ya Kitheokrasi
na Mkutano
wa Utumishi
Ij. Andiko la Siku
J1. Andiko la Siku
Huduma ya Shambani
ya Familia
(Siku ya Magazeti)
[Chati katika ukurasa wa 6]
Ratiba ya Familia
Asubuhi Alasiri Jioni
J2.
J3.
J4.
J5.
Al.
Ij.
J1.
..................................................................
Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko
la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku
Hotuba Shule ya Funzo Funzo Huduma Usomaji Tafrija
ya watu Huduma la kitabu la Fami- ya Sha- wa Biblia ya
wote na ya Kith- la Kuta- lia mbani wa Familia Familia
Funzo la eokrasi niko ya Familia
Mnara wa na Mku-
Mlinzi tano wa
Utumishi