Tulipita Kile Kiwango cha 28,500!
Mwaka wa Utumishi Wamalizika kwa Kilele Kipya Wahubiri 29,448 Wakiripoti Katika Afrika Mashariki
Mwito katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai ulikuwa “28,500!” Wahubiri 29,448 walioripoti waliitikia mwito huo. Hili ni ongezeko la wahubiri 2,096, au asilimia 7.7, zaidi ya kilele cha wakati uliopita katika Agosti 1997. Twaomba baraka zenye kuendelea za Yehova katika jitihada zetu za kutangaza Ufalme wake.
Wazee, watumishi wa huduma, na wahubiri wote vilevile wanahimizwa watafakari jitihada zilizohusika katika kufikia mradi huu. Wahubiri hao zaidi ya 29,000 wako pamoja nasi kutanikoni. Na kuna wengi zaidi ambao watakuja kila mwezi tunapoendeleza huduma yenye matokeo. Hata hivyo, mpango mzuri kwa ajili ya utumishi wa shambani, pamoja na usaidizi wenye fadhili wa kibinafsi unapohitajika, ni muhimu kwa maendeleo zaidi. Twatazamia baraka za maana sana za Yehova ili ukuzi udumishwe.—1 Kor. 3:7.
Wazee na watumishi wa huduma—hasa wale ambao ni viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko—pamoja na wahubiri wengine wakomavu na mapainia wakiendeleza jitihada ya pekee waliyoonyesha Agosti, bila shaka baraka tele za Yehova zitaonyeshwa katika ongezeko lenye kuendelea la wahubiri. Nyakati nyingine kile kinachohitajiwa tu ni kikumbusha chenye fadhili cha kushiriki katika kazi ya kuhubiri kisha labda kikumbusha kingine cha kutoa ripoti. Madokezo yaliyo katika makala ya nyongeza ya Novemba, “Uwe Mwenye Matokeo Katika Huduma Yako,” yapaswa yatusaidie kuboresha utendaji wetu na kuongeza shangwe yetu tunapoona matokeo mazuri kutokana na jitihada zetu.