Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichoorodheshwa katika barua ya Februari 5, 1998 na Mei 19, 1998 ambacho huenda kutaniko likawa nacho akibani kitatolewa kwa bei ya pekee. Makutaniko ambayo hayana ugavi wa vitabu hivyo yaweza kuomba wanavyohitaji kutoka katika ofisi ya tawi au ofisi ya nchi ya kwao. Februari: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mahali ambapo hakipatikani, toa kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Uwe na broshua Anataka kwa ajili ya watu wenye kupendezwa, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Andiko la mwaka wa 1999 ni: “Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.”—2 Kor. 6:2. Mipango yapasa kufanywa ili kuwa nalo katika Majumba ya Ufalme yetu.
◼ Kila kutaniko lilipokea fomu tatu za Orodha ya Fasihi (S-18-SW). Mwandishi wa kutaniko alipaswa kukutana na mtumishi wa fasihi na kuweka tarehe ya kuhesabu fasihi zote zilizo akibani za kutaniko mwisho wa Desemba. Hesabu kamili yapaswa kufanywa ya fasihi zote zilizo akibani, na jumla yake iingizwe kwenye fomu ya Orodha ya Fasihi. Jumla ya hesabu ya magazeti yaliyopo yaweza kupatikana kutoka kwa mtumishi wa magazeti. Tafadhali pelekeeni Sosaiti ile ya awali kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya kaboni kwa ajili ya faili zenu. Nakala ya tatu yaweza kutumiwa kufanyia kazi. Kuhesabu kwapasa kusimamiwa na mwandishi, na fomu iliyokamilishwa ichunguzwe na mwangalizi-msimamizi. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi watatia sahihi fomu hiyo.
◼ Wahubiri wote waliobatizwa watakaokuwepo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Januari 4 watapewa kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na Kadi ya Utambulishi kwa watoto wao.
◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 1, hotuba mpya ya waangalizi wa mzunguko itakuwa “Mungu Ni Halisi Kwako Kadiri Gani?”
◼ Makutaniko yapaswa kufanya mipango ya kuhudhuria Ukumbusho mwaka huu Alhamisi, Aprili 1, baada ya jua kushuka. Ingawa huenda hotuba ikaanza mapema, kupitishwa kwa mifano ya Ukumbusho hakupaswi kuanza mpaka jua lishuke. Chunguzeni kutoka vyanzo vya kwenu ili mjue jua litashuka wakati gani katika eneo lenu. Ingawa ni jambo lenye kutamanika kila kutaniko kuwa na msherehekeo wake wenyewe wa Ukumbusho, huenda hili lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au makutaniko zaidi yanaweza kutumia jengo jingine jioni hiyo. Inapowezekana, tungedokeza kuwe na angalau dakika 40 kati ya vipindi ili kuruhusu wakati kuwasalimu wageni, kutia moyo watu wapya wenye kupendezwa, na kunufaika kikamili kutokana na pindi hiyo. Baraza la wazee lapasa kuamua ni mipango gani itakayofaa kwenu.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya 1999 itatolewa Jumapili, Aprili 18. Kichwa cha hotuba hiyo kitakuwa “Urafiki wa Kweli Pamoja na Mungu na Jirani.” Muhtasari utaandaliwa. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko la mzunguko, au siku ya kusanyiko la pekee mwisho-juma huo yatakuwa na hotuba hiyo juma litakalofuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 18, 1999.
◼ Vichapo Vipya vya Braille Vinavyopatikana:
Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1999 (mabuku manne)—Gredi ya pili Kiingereza
Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1999 (buku moja)—Gredi ya pili Kiingereza
Tafadhali tia alama maombi ya vichapo vya Braille ATTENTION: BRAILLE DESK. Tia ndani jina na anwani ya mtu ambaye atatumia vifaa vya Braille.