Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Uwe na broshua Anataka kwa ajili ya watu wenye kupendezwa, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Juni: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
◼ Wahubiri wanaotaka kutumikia wakiwa mapainia-wasaidizi katika Aprili na Mei wapaswa kufanya mipango yao sasa na kuleta fomu za maombi mapema. Kufanya hivyo kutasaidia wazee wafanye mipango inayohitajiwa ya utumishi wa shambani na wawe na magazeti na fasihi za kutosha. Majina ya wote wanaopendekezwa kuwa mapainia-wasaidizi yapasa kutangaziwa kutaniko.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Jambo hili lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti inayofuata ya hesabu kusomwa.
◼ Ukumbusho utafanywa Alhamisi, Aprili 1, 1999. Ikiwa kutaniko lenu kwa kawaida huwa na mikutano Alhamisi, hiyo itafanywa siku nyingine ya juma hilo kama Jumba la Ufalme halitumiwi. Isipowezekana na Mkutano wenu wa Utumishi waathiriwa, sehemu zenye kutumika hasa kwa kutaniko lenu zaweza kutiwa ndani ya Mkutano mwingine wa Utumishi.
◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kupeleka maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haishughulikii maagizo ya fasihi ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga tangazo lifanywe kila mwezi kabla ya agizo la kila mwezi la fasihi la kutaniko halijapelekwa kwa Sosaiti ili wote wenye kupendezwa kupata fasihi ya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani ambavyo ni bidhaa za kuagizwa kipekee.