Vikumbusha vya Ukumbusho
Sherehe ya Ukumbusho mwaka huu itakuwa Alhamisi, Aprili 1. Wazee wapaswa kukazia uangalifu mambo yafuatayo:
◼ Mnapoweka saa za mkutano, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa mpaka baada ya jua kushuka.
◼ Kila mtu, kutia na msemaji, apasa kujulishwa wakati hasa na mahali pa sherehe.
◼ Mkate na divai inayofaa yapaswa kupatikana na kuwa tayari.—Ona Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1985, ukurasa wa 17.
◼ Sahani, bilauri, meza, na kitambaa cha meza kifaacho vyapasa kuletwa kwenye jumba na kuwekwa mahali pake mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkutano papasa kusafishwa kikamili mapema kabla ya wakati.
◼ Wakaribishaji na wapitishaji wa mifano wapasa kuteuliwa na kuagizwa mapema juu ya utaratibu unaofaa na wajibu wao.
◼ Mipango yapasa kufanywa kuwatumikia wowote kati ya watiwa-mafuta walio dhaifu na wale ambao hawawezi kuwapo.
◼ Makutaniko zaidi ya moja yanaporatibiwa kutumia Jumba la Ufalme lilelile, kwapaswa kuwe na makubaliano mazuri miongoni mwa makutaniko ili kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye sebule, mahali pa kuingilia, vijia vya kando ya barabara vya watu wote, na maegesho ya magari.