Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi
Juma Linaloanza Machi 1
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 17: “Ukumbusho wa Ulimwenguni Pote wa Kifo cha Kristo.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo yaliyo kwenye Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1997, ukurasa wa 11-12, fungu la 10-14. Kazia jinsi upendo mwingi wa Yehova ulivyomchochea kutuandalia fidia.
Dak. 20: Sababu Zenye Kuchochea za Kufanya Upainia-Msaidizi Katika Aprili na Mei. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi, akiwasihi wote wafikirie kwa uzito kufanya upainia-msaidizi. Pitia marekebisho ya takwa la saa kwa mapainia wa kawaida na mapainia-wasaidizi, kama ilivyoonyeshwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1999, ukurasa wa 7. Rekebisho hilo lapaswa kufanya wengi zaidi wafurahie pendeleo la utumishi wa wakati wote. Eleza jinsi ambavyo uthamini wetu kwa fidia ya Kristo hutushurutisha tujikakamue wenyewe kuhubiria wengine. (2 Kor. 5:14, 15) Mwaka huu Ukumbusho utakuwa siku ya kwanza ya Aprili. Hicho ni kichocheo kizuri kama nini kwa wahubiri wote wa Ufalme kutumia mwezi wote kuongeza utendaji wao wa utumishi! Pitia mambo makuu yaliyoteuliwa kutoka katika nyongeza za Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1997 na ya Machi 1998 zinazozungumzia utumishi wa painia-msaidizi. Fikiria njia za kujipatanisha na ratiba za mfano zilizotolewa. Pitia mipango ya utumishi ya kwenu, ambayo hutoa fursa za kutosha za kushiriki katika huduma pamoja na wengine.Watie moyo wahubiri wachukue fomu za maombi ya upainia-msaidizi baada ya mkutano.
Wimbo 44 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 20: “Waalike Waje.” Maswali na majibu. Kazia uhitaji wa kuelekeza watu wenye kupendezwa sikuzote kwenye mikutano ya kutaniko. Toa wonyesho wa mazungumzo na mtu mwenye kupendezwa, ukitumia habari iliyo katika kitabu Ujuzi, ukurasa wa 159, fungu la 20, na ukurasa wa 161-163, fungu la 5-8. Tia moyo kila mtu ajitahidi kipekee kusaidia wanafunzi wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa wahudhurie Ukumbusho Aprili 1. Onyesha nakala moja ya mwaliko uliochapwa, na ueleze jinsi unavyoweza kutumiwa kwa matokeo. Wote wanapaswa kuanza kugawanya mialiko ya Ukumbusho juma hili.
Dak. 15: “Jinsi Ambavyo Washiriki wa Familia Hushirikiana ili Kushiriki Kikamili—Katika Mikutano ya Kutaniko.” Mazungumzo yanayofanywa na kikundi cha familia. Wanapotoa maelezo juu ya mambo makuu katika makala hii, wanazungumza jinsi wanavyoweza kujitayarisha kwa ajili ya mikutano wakiwa familia. Wanazungumzia njia wanazoweza kusaidiana kushiriki na jambo ambalo lazima familia ifanye ili ifike mikutanoni kwa wakati.
Wimbo 62 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Watumishi wa Huduma Hutoa Utumishi Wenye Thamani.” Hotuba itolewe na mtumishi wa huduma mwenye uwezo. Pitia mambo makuu yaliyo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 57-59. Eleza jinsi watumishi wa huduma wanavyotumiwa kwenu kusaidia kutaniko.
Dak. 20: “Azimio Letu—Kufuatia Njia ya Yehova ya Maisha.” Hotuba. Watie moyo wote wahudhurie mikutano yote mitano ya kutaniko kwa ukawaida.
Wimbo 68 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tangaza majina ya wale watakaofanya upainia-msaidizi katika Aprili. Eleza kwamba si kuchelewa mno kuleta fomu zao za maombi. Eleza ratiba yote ya mikutano ya utumishi wa shambani iliyopangwa kwa Aprili. Tia moyo wote wafuate ratiba ya usomaji wa Biblia wa Ukumbusho ya Machi 27-Aprili 1, kama ionyeshwavyo katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1999 na kwenye 1999 Calendar.
Dak. 15: Jitayarishe kwa Ajili ya Ukumbusho. Hotuba. Wote wapaswa kufanya mipango kusaidia wanafunzi wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa wahudhurie Ukumbusho. Watu wanaohudhuria kwa mara ya kwanza huenda wasielewe ni nani anayepaswa kushiriki mifano au umaana wa sherehe hiyo. Pitia yaliyoandikwa katika Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1996, ukurasa wa 6-8, na uonyeshe jinsi tunavyoweza kusaidia mtu aliyependezwa hivi karibuni aelewe maana na kusudi la sherehe hii. Malizia kwa kupitia “Vikumbusha vya Ukumbusho” na kueleza mipango ya kwenu ya Ukumbusho.
Dak. 20: Ni Nini Hutupata Tunapokufa? Mzee azungumzia thamani na matumizi ya broshua hiyo pamoja na wahubiri wawili au watatu wenye uwezo. Tulipojifunza broshua hii katika Funzo la Biblia la Kutaniko tuliifahamu vizuri. Je, tunaitumia kwa matokeo katika utumishi wa shambani? Kikundi hicho chazungumzia yafuatayo: Kwa nini watu wengi hupendezwa na habari hii? Kinyume cha mafundisho ya dini isiyo ya kweli, ni tumaini gani ambalo broshua hii hukazia? Twaweza kutumiaje maswali yaliyo nyuma ya jalada kuchochea kupendezwa? Kuna fursa gani za kutoa broshua hii? Toa wonyesho wa utoaji mmoja ukitumia maandiko katika fungu la 14 kwenye ukurasa wa 27. Watie moyo wote wawe macho kutumia vizuri broshua hii.
Wimbo 92 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 29
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Machi. Tutatoa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Aprili. Watie moyo akina ndugu waweke fomu za kutosha za maandikisho. Huenda wengine wakaweza kupata maandikisho kazini au shuleni. Taja bei za maandikisho ziwe kama kikumbusha. Onyesha matoleo ya karibuni ya magazeti, dokeza makala ambazo zaweza kukaziwa, na utaje mambo hususa yenye kupendeza. Wote wapaswa wabebe broshua Anataka na kuitumia kuanzisha mafunzo ya Biblia na watu wenye kupendezwa.
Dak. 15: Kunufaika na Broshua Mpya, Ni Nini Hutupata Tunapokufa? Pitia mambo makuu yaliyomo ndani yake. Kama vile ambavyo tumeona tayari tulipojifunza broshua hiyo katika mafunzo yetu ya Funzo la Kitabu la Kutaniko, hiyo hutafuta asili ya fundisho la hali ya kutokufa kwa nafsi na huchunguza jinsi lilivyopata kuwa fundisho kuu la karibu dini zote ulimwenguni. Hiyo hueleza kwa njia yenye kuvutia kile ambacho Biblia husema juu ya nafsi, kwa nini sisi hufa, hali ya wafu, tumaini lililopo baada ya kifo, na kwa nini twahitaji kujua ukweli kuhusu mambo haya. Wote walifurahia kusoma broshua hii. Onyesha baadhi ya vielezi 40 na pia manukuu yaliyo mwanzoni mwa kila sehemu, yanayoweza kutumiwa kuamsha upendezi wa watu. Onyesha jinsi sehemu ya mwisho iwezavyo kutolewa unapotoa funzo la Biblia nyumbani. Waalike wahubiri watoe maelezo juu ya jinsi wanavyopanga kutumia broshua hiyo mpya katika huduma.
Dak. 18: Tuitikieje Tunaposhauriwa? Hotuba itolewe na mzee. Sisi sote tunaweza kushauriwa kuhusiana na mtazamo wetu, mwenendo wetu, mashirika yetu, au kushiriki katika utendaji wa kutaniko. Nyakati nyingine sisi huelekea kukataa shauri au kuudhika. Utayari wa kukubali na kutumia shauri waweza kuwa wa maana katika hali yetu njema ya kiroho. Pitia mambo muhimu yanayokazia sababu kwa nini twapaswa kukubali na kuthamini shauri.—Ona Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1987, ukurasa wa 27-30.
Wimbo 118 na sala ya kumalizia.