Vikumbusha vya Ukumbusho
Mwadhimisho wa Ukumbusho utakuwa Jumapili, Machi 23. Wazee wapaswa kukazia uangalifu mambo yafuatayo:
◼ Mnapoweka saa za mkutano, hakikisheni kwamba mifano itapitishwa baada ya jua kushuka.
◼ Kila mtu, kutia na msemaji, apaswa kujulishwa juu ya wakati hasa na mahali pa mwadhimisho.
◼ Mkate unaofaa na divai vyapaswa kupatikana na kuwa tayari.—Ona Mnara wa Mlinzi Machi 1, 1985, ukurasa wa 17.
◼ Sahani, bilauri, meza na kitambaa kifaacho vyapaswa kuletwa kwenye jumba na kuwekwa mahali pavyo mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkutano papaswa kusafishwa kikamili mapema kabla ya wakati.
◼ Wakaribishaji na wenye kutumikia wapaswa kuteuliwa na kuagizwa mapema juu ya utaratibu unaofaa na wajibu wao.
◼ Mipango yapaswa kufanywa kuwatumikia wale watiwa-mafuta wasiojiweza na hawawezi kuwapo.
◼ Sherehe zaidi ya moja ikiratibiwa katika Jumba la Ufalme lilelile, kwapaswa kuwe na ushirikiano mzuri miongoni mwa makutaniko ili kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye sebule, kiingilio, vijia vya kando ya barabara vya umma, na maegesho ya magari.