Vikumbusho vya Ukumbusho
Mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu utafanywa Alhamisi, Machi 28. Wazee wapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:
◼ Mnapopanga saa za mkutano, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa mpaka baada ya jua kutua.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, apaswa kujulishwa saa kamili na mahali hususa pa sherehe.
◼ Matayarisho ya mkate na divai inayofaa yapasa kufanywa mapema.—Ona Mnara wa Mlinzi, Machi, 1, 1985, ukurasa wa 17.
◼ Sahani, bilauri, meza, na kitambaa cha meza kifaacho vyapasa kuletwa kwenye jumba na kuwekwa mahali pake mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkutano huo papasa kusafishwa kabisa mapema.
◼ Wakaribishaji na watakaopitisha mifano wapasa kuteuliwa na kuelezwa mapema kuhusu wajibu wao, utaratibu utakaofuatwa, na uhitaji wa kuvalia kwa njia ya heshima.
◼ Mipango yapasa kufanywa ili kuwatumikia wowote kati ya watiwa-mafuta ambao ni wagonjwa na hawawezi kufika.
◼ Makutaniko zaidi ya moja yanapopangiwa kutumia Jumba la Ufalme lilelile, kwapaswa kuwe na makubaliano mazuri miongoni mwa makutaniko hayo ili kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye jumba, nje ya jumba, na kwenye maegesho ya magari.