Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Wahubiri wanapaswa kujulisha wenye nyumba kwamba wakipenda wanaweza kutoa mchango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. Watu wakipendezwa, toa broshua Anataka, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini? au kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa wenye nyumba wana vichapo hivyo, toa broshua inayofaa ambayo kutaniko inayo akibani.
◼ Wahubiri ambao wangependa kutumikia wakiwa mapainia-wasaidizi mwezi wa Aprili wanapaswa kufanya mipango yao sasa na kutoa ombi lao mapema. Hiyo itasaidia wazee wafanye mipango ya utumishi wa shambani na kupanga kuwe na magazeti ya kutosha na vichapo vinginevyo. Majina ya wale wote waliopendekezwa kuwa mapainia-wasaidizi yapaswa kutangaziwa kutaniko kila mwezi.
◼ Ukumbusho utafanywa Alhamisi, Machi 28, 2002. Ikiwa kutaniko lenu huwa na mikutano Alhamisi, mikutano hiyo itafanywa siku nyingine katika juma ikiwa Jumba la Ufalme halitumiwi. Ikiwa haiwezekani kufanya Mkutano wa Utumishi, sehemu ambazo zinafaa hasa kutaniko lenu zaweza kutiwa ndani ya Mkutano wa Utumishi mwingine.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla agizo la kila mwezi la kutaniko la vichapo halijapelekwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wangependa kuagiza vichapo vya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani ambavyo ni bidhaa za kuagizwa kipekee.
◼ Itafaa vikundi vya watu 20 au zaidi wanaopanga kutembelea ofisi ya tawi wawasiliane kwanza na ofisi kupitia barua. Tafadhali andikeni idadi ya watakaokuja na tarehe ya kuja. Kabla ya kuja, tafadhali pitieni Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998 kuhusu mavazi na mapambo yanayofaa mnapotembelea makao ya Betheli.
◼ Kuna hati za kisheria zinazoweza kusaidia wahubiri ambao wanahusika katika kesi za mahakamani za malezi ya watoto na haki ya kutembelea watoto zinazohusu dini yetu. Hati hizo zapasa kuombwa na baraza la wazee peke yake katika kisa ambacho ni dhahiri kwamba imani ya kidini ya mhubiri itahusika. Kwa wale wanaokabiliwa na masuala ya kawaida juu ya malezi ya watoto au haki ya kutembelea watoto, habari muhimu yaweza kupatikana katika gazeti la Amkeni! la Desemba 8, 1997, ukurasa wa 3-12; katika Amkeni! la Oktoba 22, 1988, ukurasa wa 2-14 (toleo la Kiingereza); na kwenye chati inayopatikana katika Amkeni! la Oktoba 8, 1991, ukurasa wa 9.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? (Trakti Na. 26)—Kiamhara, Kiurdu
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia—Kiganda
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko—Kiamhara
Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi —Kitigrinya
◼ Video Mpya Zinazopatikana:
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, Sehemu ya 6 —Lugha ya Ishara ya Marekani
◼ Vichapo Vipya vya Braille Vinavyopatikana:
Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? (Trakti Na. 26) (buku moja)—Kiingereza Gredi ya pili
Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha (buku moja) —Kiingereza Gredi ya pili
Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote II (mabuku manne) —Kiingereza Gredi ya pili
2002 Yearbook of Jehovah’s Witnesses (mabuku matatu) —Kiingereza Gredi ya pili
Taarifa: Vichapo vya Braille vyapasa kuagizwa kupitia kutaniko. Fomu tofauti ya Kuomba Vitabu (S-14-SW), kutia ndani jina na anwani ya msomaji huyo wa Braille yapasa kutumwa mnapoagiza vichapo vya Braille.