Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/99 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 2
  • Juma Linaloanza Agosti 9
  • Juma Linaloanza Agosti 16
  • Juma Linaloanza Agosti 23
  • Juma Linaloanza Agosti 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 8/99 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Juma Linaloanza Agosti 2

Wimbo 39

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Eleza juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Aprili ya nchi yenu na kutaniko lenu. Tia moyo wahubiri wote washiriki katika huduma ya shambani mwezi wa Agosti.

Dak. 17: “Heshimu Sana Jina Tukufu la Yehova.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Kazia maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa.—Ona kitabu Kuishi Milele, ukurasa wa 184-185.

Dak. 18: “Elimu ya Kilimwengu na Miradi Yako ya Kiroho.” Baba azungumzia makala hii na mwana wake au binti yake. Pia wanapitia habari inayohusiana na hiyo katika Amkeni!, Desemba 22, 1995, ukurasa wa 7-11.

Wimbo 148 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 9

Wimbo 138

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 12: Mapainia Wasaidia Wengine—Ni Maendeleo Gani Ambayo Yamefanywa? Hotuba na mahoji yakifanywa na mwangalizi wa utumishi. Pitia mwelekezo ulio katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1998, ukurasa wa 4. Simulia jinsi hilo lilivyopangwa kwenu, na ueleze habari ya karibuni kuhusu maendeleo ya wale waliosaidiwa. Hoji painia mmoja au wawili na wahubiri fulani ambao wamenufaika na msaada wao. Tia moyo wale wanaofuata kusaidiwa watumie ifaavyo uandalizi huo.

Dak. 25: “Je, Wewe Umefunguliwa Mlango wa Upainia Sasa?” Mazungumzo ya maswali na majibu yakiongozwa na mzee. Kwa njia yenye kutia moyo, onyesha uwezekano uliopo kwa wahubiri wengi kupainia. Hoji mapainia wanaoweza kusimulia mambo yao wenyewe yaliyoonwa ya jinsi walivyoweza kushinda vizuizi vya kawaida na kufanikiwa. Changanua “Ratiba za Mfano za Painia wa Kawaida,” ukikazia jinsi ambavyo mpango mzuri unavyoweza kufanya takwa la saa lifikiwe. Tangaza kwamba yeyote anayetaka fomu ya ombi la painia anaweza kuipata baada ya mkutano.

Wimbo 202 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 16

Wimbo 131

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ni miisho-juma miwili tu iliyobaki ya Agosti, kwa hiyo, tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma kabla ya mwisho wa mwezi. Pitia “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.”

Dak. 15: “Twapaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1997. Taja kwamba hivi karibuni utendaji wa kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani umepungua. Watu katika eneo letu wangali wanapendezwa. Twapaswa kujitahidi sana kuwasaidia.

Dak. 20: Je, Unashiriki Katika Kufanya Wanafunzi? Mazungumzo na wasikilizaji. Kwa sababu ya fasihi nyingi zinazoangushwa, lengo letu lapasa liwe kuanzisha mafunzo ya Biblia ili tuweze kusaidia watu wanufaike na vichapo wanavyopokea. Omba wahubiri watoe maelezo kuhusu matatizo yanayowazuia wasiongoze mafunzo zaidi: (1) Ni vigumu kupata watu wanaotaka kujifunza. (2) Watu fulani wanaoonyesha kupendezwa husema kwamba wana shughuli nyingi mno wasiweze kujifunza. (3) Baada ya funzo kuanzishwa, ni vigumu kumpata mtu nyumbani ili kuendeleza funzo kwa ukawaida. Pia zungumzia hisia ambazo huenda wahubiri wakawa nazo kuhusu kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia: (1) ‘Sihisi kuwa nastahili kuwa mwalimu.’ (2) ‘Sina wakati wa kuongoza funzo kila juma.’ (3) ‘Mimi husita kuwa na wajibu kuelekea mtu mwingine.’ (4) ‘Naridhika na kushiriki sehemu zile nyingine za huduma.’ Toa madokezo yafaayo ya jinsi ya kushinda vizuizi hivi ili wewe binafsi ushiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi. Panga wahubiri wenye mafanikio wasimulie shangwe ambayo wamepata katika kuongoza mafunzo ya Biblia.—Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1998, fungu la 3-8, 15.

Wimbo 100 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 23

Wimbo 94

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Saidia Wapya Wanaopendezwa Wathamini Utakatifu wa Ndoa. Mzee azungumza na wasikilizaji kwa kutegemea kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 241-243. Sisi hukuta wenzi wanaokubali ujumbe wa Ufalme lakini wanafanya maendeleo polepole kwa sababu wanaishi pamoja bila kufunga ndoa kisheria. Zungumzia jinsi ya kuwasaidia waelewe sababu inayofanya iwe lazima kwa Wakristo kuwa na ndoa yenye kuheshimika. (Ona Amkeni!, Novemba 8, 1992, ukurasa wa 28-29.) Toa madokezo ya kile tunachoweza kusema kwa busara ili kusaidia wenzi hao waone kwa nini hawawezi kuwa sehemu ya kutaniko mpaka wahalalishe kisheria ndoa yao.

Dak. 20: “Utamwambia Nini Mbudha?” Maswali na majibu. Katika maeneo ambayo hakuna Wabudha, tumia wakati huo kuzungumzia mahitaji ya kwenu. Mara nyingi sisi hujiuliza tuseme nini tunapopata watu katika eneo wanaodai kuwa wafuasi wa dini isiyo ya Kikristo ambayo ina mawazo, mazoea na desturi za kigeni kwetu. Makala hii yaanza mfululizo wa sehemu tano kuhusu habari hii. Toa wonyesho wa utoaji uliotayarishwa vizuri. Ili upate habari zaidi kuhusu Ubudha, ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1998; kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 21; na kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura ya 6.

Wimbo 133 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 30

Wimbo 99

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Agosti. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wapaswa kuangalia kwamba kila mtu katika kikundi chao ametoa ripoti ili ripoti zote zihesabiwe kufikia Septemba 6.

Dak. 17: Twapenda Ndugu Zetu. Hotuba itolewe na mzee, kutia ndani mazungumzo na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi, Desemba 1, 1995, ukurasa wa 15-17, fungu la 7-11. Kazia manufaa ambazo sote tunapata tunapojua ndugu zetu vizuri, tunapotiana moyo, na kusaidiana kuvumilia majaribu. Toa dokezo la jinsi inavyowezekana kufanya hivyo zaidi. Omba wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa kuonyesha jinsi walivyochangamshwa na kuimarishwa na kitia-moyo chenye upendo cha wengine.

Dak. 18: Toa Sababu ya Tumaini Lako. Mzee anahoji tineja mmoja au wawili wenye kielelezo chema ambao wako shuleni. Wanakabiliwa daima na hali ambazo marika walimwengu wanataka kujua sababu inayofanya matineja wetu wasijiunge na shughuli zao. Ingawa wanatwaa fursa hizo kueleza masadikisho yao yanayotegemea Biblia, vijana wetu wanahitaji kuwa imara katika kustahimili mkazo wao. Kikundi hicho chazungumzia jinsi wanavyoweza kuitikia wanapopewa tumbaku au dawa za kulevya. Pitia hoja zinazotolewa katika kitabu Vijana Huuliza, ukurasa wa 277-281. Eleza jinsi kutetea azimio lao la kufanya yaliyo sawa huwa ulinzi na kutoa ushahidi mzuri.

Wimbo 129 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki