Habari Za Kitheokrasi
Romania: Maongezeko mazuri yalionekana katika utendaji wa painia na idadi ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa, kukiwa na kilele kipya cha wahubiri 37,502 shambani mwezi wa Februari.
Rwanda: Kampeni ya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme katika Rwanda yaendelea vizuri. Kufikia mwezi wa Juni 1999, Majumba ya Ufalme 16 yaliwekwa wakfu. Mengi ya majumba hayo yameripotiwa kwenye Huduma ya Ufalme Yetu kwenye Habari za Kitheokrasi kuanzia toleo la Januari 1998 hadi toleo la Agosti 1999. Majumba ya Ufalme yafuatayo ni miongoni mwa yale 16 yaliyowekwa wakfu: Butare, Kigali Sud, Matyazo, Nyakinama, Rebero na Shaki.
Visiwa vya Marshall: Mwezi wa Februari kulikuwa na jumla ya wahubiri 203—ongezeko la asilimia 4 zaidi ya mwezi wa Februari mwaka uliopita!