Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
Juma Linaloanza Oktoba 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 17: “Neno la Mungu la Kiunabii Litatimia Lote!” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatie kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Taja mambo machache kutoka katika kitabu kipya yanayokazia umaana wa nyakati zetu.
Dak. 18: Kazia Uangalifu Magazeti! Taja jumla ya magazeti yaliyoangushwa na kutaniko mwezi jana. Hiyo yalinganaje na idadi iliyopokewa kutoka kwa Sosaiti? Ikiwa kuna tofauti kubwa, ni nini kinachohitaji kufanywa? Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu mambo yafuatayo: (1) Kila mhubiri apaswa kuagiza kiwango cha magazeti cha kutosha lakini kinachofaa. (2) Ione kila Jumamosi kuwa Siku ya Magazeti. (3) Panga ratiba yako ya utumishi itie ndani utendaji wa magazeti kila mwezi. (4) Panga kutoa ushahidi wa vivi hivi zaidi ukitumia magazeti kuanzisha mazungumzo. (5) Wapelekee wafanya-biashara na wataalamu makala za pekee ambazo yaelekea watapendezwa nazo. (6) Andika maandishi sahihi ya maangusho, na usitawishe njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida, ukirudi kwa ukawaida na matoleo ya karibuni. (7) Tumia vizuri magazeti ya zamani ili yasirundamane. Onyesha magazeti ya karibuni, na utaje makala ambazo labda zitachochea kupendezwa. Panga mtu mzima na kijana watoe wonyesho kila mmoja akitoa onyesho fupi la utoaji wa magazeti.—Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1995.
Wimbo 105 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Habari za Kitheokrasi na Kikumbusha Chenye Msaada.
Dak. 20: “Jinsi ya Kupata Shangwe Zaidi Kutokana na Mikutano.” Maswali na majibu. Taja mifano hususa ya jinsi tunavyoweza kuonyesha tunajali na kutiana moyo mikutanoni. Omba wasikilizaji wasimulie mifano kutokana na mambo yao wenyewe yaliyoonwa.
Wimbo 152 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa ya utumishi wa shambani.
Dak. 13: “Je, Unahama?” Hotuba yenye kutia moyo itolewe na mwandishi. Wahubiri wakiona kuwa lazima kuhamia kutaniko jingine, ni jambo la maana wazoee mazingira yao mapya ili waepuke kurudi nyuma kiroho. Kazia uhitaji wa kujulisha wazee mipango hiyo na kuwaomba msaada wa kuwasiliana na kutaniko jipya.
Dak. 22: “Kufanya Wanafunzi Miongoni Mwa Jirani Zetu Waasia.” Maswali na majibu. Taja sehemu ambazo huenda tukakubaliana na Mwasia. Toa wonyesho uliotayarishwa vizuri. Taja kwamba Waasia wengi huandikisha magazeti yetu.
Wimbo 142 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 25
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Saidia wote wajitayarishe kutoa broshua Anataka au kitabu Ujuzi mwezi wa Novemba. Eleza jinsi ya kutayarisha utoaji unaokazia swali hili, “Je, Mungu hujibu sala?” Tumia mambo yaliyo katika somo la 7 katika broshua au sura ya 16, fungu la 12-14, katika kitabu. Toa wonyesho mfupi unaotia ndani andiko moja.
Dak. 15: Kupata Majibu ya Maswali ya Biblia. Mtumishi wa huduma afikiwa na mhubiri ambaye amekutana na mtu mwenye kupendezwa mwenye swali la Biblia. Badala ya kumpa jibu, mtumishi wa huduma anamweleza jinsi ya kulipata. Kwanza, apitia madokezo yapatikanayo katika kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 7, fungu la 8-9. Kisha, wakiwa pamoja wanafanya utafiti wa swali ambalo mara nyingi huulizwa katika eneo la kwao. Wanachunguza marejezo hususa yanayoshughulika na somo hilo na kupata mambo yenye kusadikisha ambayo yanaelewesha sababu ya msingi ya jibu la Biblia. Tia moyo wasikilizaji wafanye aina hii ya funzo lenye kuthawabisha ili kufanya utafiti wa maswali ya Biblia.
Dak. 15: Miradi Tuwezayo Kuweka. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Pitia miradi yenye kutumika inayoonyeshwa kwenye sanduku lililo kwenye ukurasa wa 11 wa Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 1997. Tia ndani kitia-moyo cha kushiriki katika utumishi wa painia-msaidizi au painia wa kawaida. Eleza jinsi kufikia miradi hiyo kunavyoweza kutunufaisha kibinafsi. Waalike wasikilizaji wasimulie baadhi ya shangwe walizopata walipoweza kufikia miradi fulani ya kitheokrasi.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.