Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/99 uku. 1
  • Neno la Mungu la Kiunabii Litatimia Lote!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Neno la Mungu la Kiunabii Litatimia Lote!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Mamilioni Watahudhuria—Namna Gani Wewe?
    Amkeni!—1999
  • Neno la Mungu la Kiunabii Hutoa Tumaini kwa Wakati Ujao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Uwe na Imani Katika Neno la Mungu la Kiunabii!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • “Hofu ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya Umekaribia
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 10/99 uku. 1

Neno la Mungu la Kiunabii Litatimia Lote!

1 Mashahidi wa Yehova sikuzote wamependezwa na unabii wa Biblia. Kwa hiyo, tulisisimuka kujua kwamba kichwa cha mkusanyiko wa wilaya wa mwaka huu kingekuwa “Neno la Mungu la Kiunabii.” Tulikuwa na hamu sana ya kujua kile ambacho Yehova alikuwa ametuandalia kikiwa ‘chakula kwa wakati ufaao.’ (Mt. 24:45) Yeye hakututamausha.

2 Mambo Makuu ya Mkusanyiko: Hotuba ya msingi ya Ijumaa, “Sikiliza Neno la Mungu la Kiunabii,” ilitia ndani mazungumzo yenye kuelimisha ya simulizi la mgeuko-umbo. (Mt. 17:1-9) Ilikazia kwamba hivi sasa tuko ukingoni mwa nyakati nzuri kwa sababu tuko katika wakati wa mwisho kabisa, mfumo mpya ukiwa karibu sana! Njia ya maana tuwezayo kusikiliza Neno la Mungu ni kwa kulisoma kwa ukawaida. Ule mfululizo “Pendezwa na Kusoma Neno la Mungu” uliandaa madokezo yenye kutumika ya kufanya usomaji wetu wa Biblia uwe na faida zaidi na wenye kufurahisha.

3 Jumamosi alasiri tulichunguza sababu ambazo twapasa kusadikishwa kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Je, unaweza kukumbuka yote hayo? Jumapili asubuhi, unabii wa Habakuki ulitokezwa kwa njia yenye kupendeza tulipojifunza kwamba siku yetu hufanana sana na siku yake na kwamba hivi karibuni matukio ya maana sana yatatukia wakati Yehova atakapoharibu waovu na kuokoa waadilifu. Je, ulielewa jambo kuu la drama ya Biblia juu ya Yakobo na Esau? Lazima tutafute kwa bidii baraka kutoka kwa Yehova, tukikinza roho ya ubaridi.

4 Kitabu Kipya Chenye Kuvutia Sana: Tulisisimuka kama nini tulipopokea kitabu kipya, Sikiliza Unabii wa Danieli! Bila shaka unasoma kichapo hiki chenye kuvutia sana. Msemaji aliyekitoa alisema: “Isipokuwa mambo machache, unabii wote ulio katika kitabu cha Danieli umetimizwa.” Je, hilo halikazii uharaka wa nyakati zetu?

5 Programu ya mkusanyiko imeimarisha usadikisho wetu kwelikweli kwamba ahadi zote za Mungu ambazo hazijatimizwa zitatimia. Tunachochewa twendelee kuwatangazia wengine neno la Mungu la kiunabii!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki