Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/99 uku. 7
  • Je, Unahama?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unahama?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Kukabiliana na Changamoto ya Kuhamia Kutaniko Jipya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Kutaniko na Lijengwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kutaniko na Limsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 10/99 uku. 7

Je, Unahama?

Ikiwa jibu la swali hilo ni ndiyo, kuna mambo mengi ambayo wewe na wengine mwahitaji kuchukua hatua kuyafanya. Kwa kufuata hatua za msingi zilizoorodheshwa hapa chini, utakuwa umejiimarisha katika kutaniko lako jipya.

(1) Mara unapojua uendako, mwandishi wa kutaniko lako la sasa anaweza kupata anwani ya Jumba la Ufalme la kutaniko lako jipya. Unapofika sehemu hiyo, tafuta Jumba la Ufalme mara moja na uhakikishe umejua saa za mikutano ya kutaniko. Ikiwa makutaniko zaidi ya moja yanatumia Jumba lilelile la Ufalme, uliza wazee wakuambie unaishi katika eneo la kutaniko jipi. Usichelewe kuhudhuria mikutano na kufahamiana na wazee wa hapo.

(2) Mwandishi wa kutaniko lako la sasa na yule wa kutaniko lako jipya watashirikiana kuhamisha kadi yako na za familia yako za Rekodi ya Kutaniko Kuhusu Mhubiri. Barua ya utambulisho pia itapelekewa wazee wa kutaniko lako jipya. (Ona Sanduku la Swali la Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1991.) Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ya hapo yapaswa kumjulisha kiongozi wa funzo la kitabu anayehusika kuhusu kufika kwako ili aweze kuwasiliana nawe na kukusaidia ujue mahali pa kikundi chako kipya cha funzo la kitabu.—Rom. 15:7.

(3) Wahubiri wote katika kutaniko lako jipya wana shangwe ya kutimiza fungu fulani—lile la kufahamiana nawe na kukukaribisha. (Linganisha 3 Yohana 8.) Bila shaka, hilo lamaanisha lazima uwepo kwenye mikutano ili uweze kufurahia kitia-moyo na badilishano lenye kujenga pamoja na ndugu na dada zako.

(4) Wewe haupaswi kungoja hadi kazi yote ya kuhama ikamilike kabla ya kushiriki katika huduma ya shambani pamoja na kutaniko lako jipya. Ukitanguliza masilahi ya Ufalme, mambo mengine yatashughulikiwa, nawe utahisi starehe sana katika mazingira yako mapya. (Mt. 6:33) Unapotulia katika makao yako mapya, yaelekea utataka kualika wengine katika kutaniko wakutembelee ili mfahamiane.—Rom. 12:13b.

Kuhama ni mradi mkubwa. Hata hivyo, kila mmoja anayehusika akifanya yanayopendekezwa, hakutakuwa na hali ya kurudi nyuma kiroho. Wote watavutiwa na udugu wetu wenye upendo wa Kikristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki