Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/99 uku. 1
  • Jinsi ya Kupata Shangwe Zaidi Kutokana na Mikutano

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kupata Shangwe Zaidi Kutokana na Mikutano
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Je, Unashiriki Katika Kufanya Mikutano ya Kikristo Iwe Yenye Kujenga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mikutano Hunufaisha Vijana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Desturi Yako Ni Nini?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 10/99 uku. 1

Jinsi ya Kupata Shangwe Zaidi Kutokana na Mikutano

1 Mikutano ni ya maana kwa hali yetu njema ya kiroho. Shangwe tupatayo kutokana nayo yahusiana moja kwa moja na yale tunayofanya kabla, wakati wa mikutano, na baada ya hapo. Twaweza kujisaidiaje sisi wenyewe na wengine kuendeleza shangwe kubwa ya kuhudhuria mikutano?

2 Kabla ya Mikutano: Kutayarisha huwa na matokeo katika kupata shangwe kutokana na mikutano. Tunapokuwa tumejitayarisha vizuri, sisi huwa na mwelekeo wa kusikiliza kwa makini na kushiriki. Kwa kuongezea, mgawo wowote tunaopokea wapasa kutayarishwa vizuri tukiwa na lengo la kutoa habari hiyo kwa usahihi kulingana na maagizo na kuvutia upendezi wa wasikilizaji. Twapaswa kujizoeza vizuri kabisa. Tunapochangia kwenye mikutano yenye uchangamfu na yenye kujenga inayofaidi kila mtu, maendeleo yetu binafsi huwa dhahiri nasi hupata shangwe kubwa zaidi.—1 Tim. 4:15, 16.

3 Wakati wa Mikutano: Kutoa maelezo mikutanoni kwaweza kutusaidia tuifurahie zaidi. Sehemu ambazo huhitaji wasikilizaji washiriki zapasa kuonwa kuwa migawo ya kibinafsi kwa kila mtu kutanikoni. Maelezo ambayo ni mafupi na yenye kulenga kichwa cha msumari mara nyingi huwa na matokeo zaidi. Kusimulia kifupi mambo yaliyoonwa kwaweza kutia moyo sana na kuchochea, nasi twapaswa kuwa macho kutia ndani mambo hayo inapofaa. (Mit. 15:23; Mdo. 15:3) Tunapokuwa na sehemu mkutanoni, twapaswa kuongea kwa uchangamfu na usadikisho, tukifanya iwe yenye kupendeza, halisi, na yenye kutumika.

4 Baada ya Mikutano: Kushiriki na wengine neno lenye fadhili, salamu ya kirafiki, na mambo makuu machache yaliyozungumziwa mikutanoni, kutatufaidi sote. Kuonyesha shangwe yetu tunapowaona vijana, wazee, na wapya wakishiriki, huongeza upendo wa udugu. Badala ya kuongea isivyofaa kuhusu watu fulani ambao huenda wakakosa mikutano, twapaswa kushiriki nao shangwe itokanayo na kuihudhuria, hivyo tukiwatia moyo wahudhurie.—Ebr. 10:24, 25.

5 Acheni tusijinyime uandalizi huo wa kubadilishana kitia-moyo. (Rom. 1:11, 12) Kwa kudhamiria kufanya jitihada yote, sote twaweza kudumisha shangwe katika kuhudhuria mikutano ya Kikristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki