Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/99 uku. 8
  • Kufanya Wanafunzi Miongoni mwa Jirani Zetu Waasia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufanya Wanafunzi Miongoni mwa Jirani Zetu Waasia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 10/99 uku. 8

Kufanya Wanafunzi Miongoni mwa Jirani Zetu Waasia

1 “PANUKA KABISA”!—Sitawisha Bidii ya Kimishonari: Watu wengi wa asili ya Asia huishi Mashariki mwa Afrika. Wengi wao walitoka katika bara kubwa la India lakini hatimaye idadi kubwa mno wamezaliwa Afrika Mashariki. Wao wanatoka hasa katika malezi ya Kihindu, Kikalasinga, au Kiislamu.

2 Sasa tuna Mashahidi na wanafunzi wa Biblia kadhaa wasemao Kipunjabi, Kigujarati, na Kihindi. Mengi kati ya majiji na miji yetu ina jamii nyingi za Kiasia, lakini makutaniko ya mashambani pia yana maduka au mikahawa ya Waasia. Tuna pendeleo na daraka la kufanya wanafunzi miongoni mwa jirani zetu Waasia, popote pale ambapo huenda wakapatikana kupatana na amri ya Yesu. (Mt. 28:19, 20) Je, utasaidia katika mavuno ya shamba hili?—Mt. 9:37, 38; Yn. 4:35.

3 Ni jambo la asili kuhisi kuwa hatufai tunapotolea ushahidi watu ambao lugha, dini, na utamaduni wao ni wa kigeni kwetu. Hata hivyo, wengi wa wahubiri wetu Waasia wamesaidiwa kujua kweli na Mashahidi kutoka malezi yasiyo ya Kiasia. Lazima tukumbuke kwamba ni Yehova ambaye hutufanya tustahili katika kazi yake.—2 Kor. 3:5.

4 Basi, ni nini ulio ufunguo wa mafanikio kwa huduma hii ya “kigeni?” Ni upendo ulioenea, ulio mkamilifu kwa watu wa jamii zote mioyo yetu ‘inapopanuka kabisa’! (2 Kor. 6:11-13) Upendo huo wa Kikristo husitawisha bidii ya kimishonari na roho kama ya Kristo katika kushughulika na hali njema ya wengine.—Flp. 2:1-4.

5 Mtume Paulo, alipokuwa Athene, hakutazama tu ‘vitu vya kupewa heshima’ vilivyokuwa mahali alipokuwa. Badala yake, ‘alivitazama kwa uangalifu.’ (Mdo. 17:23) Ili tuwe waeneza-evanjeli wenye matokeo, twahitaji kufanya vivyo hivyo. Tunapofikia nyumba ambayo familia ya Kiasia huishi, twapaswa kuangalia nini ili tujifunze jambo fulani kuhusu dini ya mwenye nyumba? Kwa mfano:

◼ Nyumba ya Kalasinga: Huenda ikajulikana kwa kibandiko cha karatasi kilicho na maandishi ya Kipunjabi au ishara, nishan sahib, upanga ukatao kuwili ulio ndani ya mviringo, uliozingirwa na panga mbili zilizojipinda. Ndani ya nyumba, picha za guru na Hekalu la Dhahabu katika Amritsar zaweza kuonekana.

◼ Mlangoni pa Mhindu: Paweza kuwa na ishara ya swastika au nazi kwenye ngazi ya mlangoni. Huenda pia kukawa na safu ya majani ya mwembe au kibandiko (chenye ishara ya Om) juu ya mlango wa mbele.

6 Twaweza kujitayarishaje kuwahubiri Wahindu na Makalasinga? Kwa kuzoelea sana habari iliyo katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, Sura ya 5: “Uhindu Jitihada ya Kutafuta Kukombolewa.” Ona jinsi sura hii hutufahamisha maoni ya dini ya Hindu kuhusu: Mungu (fu. 27-32); Maandishi matakatifu (fu. 10-14); Aina za ibada (uku. wa 110); Kusudi la uhai (fu. 24); Hali ya wafu (fu. 39-43); Kuteseka kwa binadamu (fu. 21-23). Itikadi kuu za Makalasinga zaonyeshwa katika ukurasa wa 100-101. Tunapoelewa jambo fulani kuhusu maandishi na desturi za dini ya Hindu, huenda tukatumia ujuzi wetu wa kuwafikia mara ya kwanza ukiwa daraja la kuwasaidia wasababu kwa kutumia Biblia, namna mtume Paulo alivyofanya.—Mdo. 17:22-31.

7 Unapotembelea nyumba za Waasia, kwanza jaribu kuongea na kichwa cha familia. Ukiweza kufanya hivyo, huenda akaita washiriki wale wengine wa familia wajiunge na mazungumzo.—Linganisha Matendo 16:32.

Salamu ya Msingi ya Kipunjabi

Sat Siri Akal, Ki Haal Hai?

(“Kweli hudumu milele, U hali gani?”)

Salamu ya Msingi ya Kigujarati

Kem Chho?

(“U hali gani?”)

◼ Ukikaribishwa, uwe mwangalifu kutotumia fursa hiyo kupita kiasi, au kukaa sana.—Linganisha Mithali 25:17.

◼ Ili kuanzisha mazungumzo na Waasia wa umri mbalimbali, tumia utangulizi unaopatikana kwenye ukurasa wa 9-15, wa kitabu Kutoa Sababu:

Wazee-wazee: Uhalifu/Kutopatwa na Madhara; Upendo/Fadhili; Uzee/Kifo

Wazazi: Jamaa/Watoto; Maisha/Furaha

Vijana: Kazi ya Kuajiriwa/Nyumba; Udhalimu/Kuteseka

◼ Msaada wa Kushughulika na vipingamizi vya kawaida waweza pia kupatikana katika kitabu Kutoa Sababu chini ya vichwa vifuatavyo:

Biblia: Ukurasa wa 48—‘Biblia ni kitabu cha watu weupe.’

Ajali: Ukurasa wa 27—Je! kila mtu ameamuliwa kimbele “wakati wa kufa”?

Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine: Ukurasa wa 158—‘Mimi naitikadi kuna kuzaliwa upya katika mwili mwingine.’

Dini: Ukurasa wa 69—Je! inafaa mtu kuacha dini ya wazazi wake?

8 Twataka watu katika eneo letu waone kwa upande wetu uchangamfu na kupendezwa ambako Yesu Kristo alionyesha katika huduma yake. Twahitaji kuonyesha uchangamfu huo nyakati zote! Hata kama wale tunaoongea nao wanaonyesha kupendezwa kidogo na ujumbe wetu, wazo tutakaloacha litafanya iwe rahisi zaidi kwa Shahidi atakayewatembelea baadaye.

9 Ujumbe wa Kikristo ni wenye nguvu sana. Unaweza kupindua “mawazowazo na kila jambo lililoinuka sana lililoinuliwa dhidi ya ujuzi wa Mungu.” (2 Kor. 10:4, 5) Lakini tunapotolea ushahidi wale ambao imani yao haitegemei Biblia twahitaji kuwa na ujuzi wa msingi wa itikadi na mafundisho yao ili kutuwezesha kuwavuta kwa Neno la Yehova. Kwa kufanya hivyo ndipo tu tuwezapo kufanya wanafunzi. Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu chaweza kutusaidia kwa habari hiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki