Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pitio la vitabu vikiwa vimefungwa kuhusu habari iliyozungumziwa katika migawo ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwa juma la Januari 3 hadi Aprili 17, 2000. Tumia karatasi tofauti kuandika majibu kwa maswali mengi kadiri uwezavyo kwa wakati uliogawiwa.
[Taarifa: Wakati wa pitio la kuandika, ni Biblia pekee inayoweza kutumiwa kujibu swali lolote. Marejezo yanayofuata maswali ni kwa ajili ya utafiti wako wa kibinafsi. Nambari za ukurasa na fungu huenda zisipatikane katika marejezo yote kwenye Mnara wa Mlinzi.]
Jibu kila ya taarifa zifuatazo Kweli au Si Kweli:
1. Nyakati nyingine lazima tungojee kupokea baraka za Yehova, kwa kuwa Yehova anajua hali yetu na huandaa kila uhitaji wakati ambapo utatufaa zaidi. (Zab. 145:16; Yak. 1:17) [w98-SW 1/1 uku. 23 fu. 6] Kweli.
2. Leo twategemezwa kiroho kwa kusoma tu maneno ya Yehova. (Kum. 8:3) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w86-SW 2/1 uku. 30 fu. 15, 17.] Kweli. Muktadha wa Kumbukumbu la Torati 8:3 huonyesha kwamba lazima tuwe tukifanya mapenzi ya Mungu ili kuona njia nzuri ajabu ambayo Yehova anashughulika nasi na kutenda kwa ajili yetu. (Linganisha Zaburi 34:8; Yohana 4:34.)
3. Kanuni iliyokaziwa katika Sheria ya Kimusa kwenye Kumbukumbu la Torati 23:20 yaonyesha kwamba si jambo lenye upendo kwa Mkristo kutaka riba anapokopesha pesa. [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w86-SW 10/15 uku. 12 fu. 9.] Si Kweli. Si kosa kuomba riba wakati unapokopesha pesa kwa makusudi ya biashara.
4. Ripoti ya kutazamia mema ya Yoshua na Kalebu ilitegemea imani yao thabiti katika nguvu na azimio la Waisraeli kushinda vizuizi vyovyote ambavyo viliwazuia kuchukua Bara Lililoahidiwa. (Hes. 13:30) [w98-SW 2/1 uku. 5 fu. 4] Si Kweli. Mtazamo wao na ripoti yao zilionyesha kuwa kwao na uhakika kamili katika uwezo wa Yehova wa kutimiza neno lake la kuwapa Bara Lililoahidiwa.
5. Akiirejezea “zawadi” katika 1 Timotheo, Paulo alikuwa akimkumbusha Timotheo kutiwa kwake mafuta kwa roho takatifu na zawadi ya kimbingu ambayo ilikuwa ikimngojea. (1 Tim. 4:14) [w98-SW 2/15 uku. 25 fu. 1] Si Kweli. Mstari wa 13 na 16 wa sura hiyohiyo waonyesha kwamba Paulo alikuwa akimkumbusha Timotheo juu ya pendeleo lake la utumishi na uhitaji wa kulishughulikia kwa kuwajibika.
6. Kitabu cha Yoshua hakiandai uhusiano wowote wa maana katika rekodi inayoongoza kwenye kutokezwa kwa Mbegu ya Ufalme. [si-SW uku. 46 fu. 24] Si Kweli. Kama ionyeshwavyo na Mathayo 1:5, Rahabu, anayefafanuliwa katika kitabu cha Yoshua, alikuja kuwa nyanya ya Yesu Kristo.
7. Kitabu cha Waamuzi ni rekodi ya wanaume walioteuliwa na kuwekwa rasmi na Israeli kutawala taifa kabla ya wakati wa wafalme. [si-SW uku. 46 fu. 2] Si Kweli. Wanaume hao waliinuliwa na Yehova ili kukomboa watu wake kutoka utumwa wa kigeni.
8. Ombi la Gideoni, kama lifafanuliwavyo kwenye Waamuzi 6:37-39, laonyesha kwamba alikuwa mwenye hadhari na kutilia shaka kupita kiasi. [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w88-SW 4/1 uku. 30 fu. 5.] Si Kweli. Gideoni alitaka kuwa na uhakika kwamba msimamo wake ulifaa. Kwa kuwa hakuwa na Neno la Mungu lililoandikwa kama sisi tulivyo nalo, hiyo ilikuwa ndiyo njia yenye matokeo mazuri kuhakikisha jambo hilo.
9. Kwa kuwaagiza wanafunzi wake ‘wasimkumbatie yeyote katika salamu barabarani,’ Yesu alikuwa akikazia uharaka wa kazi ya kuhubiri na uhitaji wa kukazia uangalifu zaidi mgawo huu wenye maana zaidi. (Luka 10:4) [w98-SW 3/1 uku. 30 fu. 5] Kweli.
Jibu maswali yafuatayo:
10. Kwa nini ni muhimu kwa maneno ya Yehova yathibitike kuwa kwenye mioyo ya wazazi? (Kum. 6:5, 6) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w98-SW 6/1 uku. 20 fu. 4.] Ndipo tu wangeweza kukaza kikiki kwa matokeo maneno ya mafundisho ya Yehova ndani ya watoto wao. (Kum. 6:7; 11:19)
11. Kichwa cha familia anawezaje kutumia kanuni iliyoandikwa kwenye Kumbukumbu la Torati 11:18, 19? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona fy-SW uku. 70 fu. 14.] Kwa kuwa chonjo sikuzote kutafuta fursa za kujenga mtazamo wa kiroho wa familia yake, akitambua kwamba funzo la familia si pindi pekee ya kuwasilisha mambo yaliyo ya maana kiroho.
12. Ni dokezo gani la Kimaandiko linaloonyesha kwamba mtumwa aliyetoroka Onesimo yaelekea alikuwa na mtume Paulo kwa muda fulani kabla ya Paulo kumwandikia Filemoni? [w98-SW 1/15 uku. 30 fu. 2] Onesimo alikuwa amekuwa na Paulo kwa muda wa kutosha kwa Paulo kusema hivi kumhusu “ndugu yangu mwaminifu na mpendwa.” (Kol. 4:9)
13. Tuonapo ukosefu wa haki au kupatwa nao sisi wenyewe, twaweza kufanya nini ili kuepuka mtazamo wa kukata tamaa au wa kutazamia mabaya? [w98-SW 2/1 uku. 6 fu. 2-3] Twaweza kukumbuka kwamba waovu wataadhibiwa kwa wakati ambao Mungu ameuweka; pia, twaweza kuendelea kufanya yaliyo mema na kumngojea Yehova, ambaye “hawaachi watauwa wake.” (Zab. 37:28, 29)
14. Yoshua na Gideoni walionyeshaje staha ya hali ya juu kwa sheria ya Mungu? (Kum. 20:8, 15-18) [si-SW uku. 41 fu. 32] Yoshua ni kielelezo bora cha utii katika kutekeleza ushindi wa Bara Lililoahidiwa na kutochukua nyara yoyote (Yos. 8:24-27); kuondoa kwa Gideoni wale wenye kuogopa na kutetemeka kutoka kwenye jeshi lake kulikuwa ni kutii Sheria. (Amu. 7:1-11)
15. Matukio yanayofafanuliwa kwenye Yoshua 10:10-14 yanalinganaje na yale yanayoweza kutazamiwa kwenye Har–Magedoni? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w86-SW 12/15 uku. 23 fu. 12–uku. 24 fu. 14.] Yehova atashinda mataifa yaliyoungana pamoja dhidi ya Ufalme na waungaji-mkono wake kwa kuwavuruga mbele ya majeshi yake yenye kuua; pia kwa njia ya mwujiza atatumia nguvu za asili kama silaha.
16. Taja manufaa tatu za kusifu kwa moyo mweupe mwenendo unaostahili. (Linganisha Mithali 15:23.) [w98-SW 2/1 uku. 31 fu. 5-6] Huchangia kuthaminiana kwa njia yenye uchangamshi na yenye kujenga. Hutia moyo kujitahidi kufikia miradi yenye kustahili sifa. Hutufanya tutake kufanya kazi kwa bidii. Huenda ikasaidia kufanyiza utu wetu huku tukikusudia kuishi kulingana na viwango vitarajiwavyo kwetu.
17. Kupatana na Yoshua 20:4, mtu anaweza kukimbiaje kwenye jiji la makimbilio la kitamathali? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w86-SW 12/15 uku. 24 fu. 16.] Mtu hukimbilia huko kwa kuchukua hatua kupata dhamiri safi mbele za Mungu; hatua hizo zatia ndani kuungama dhambi, kutubu, kugeuka, kujiweka wakfu kwa Mungu, na kubatizwa katika maji.
18. Twaweza kuonyeshaje heshima kwa kanuni ya maneno “kila mtu mahali pake,” kama ilivyorekodiwa kwenye Waamuzi 7:21? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w82-SW 11/1 uku. 21 fu. 17.] Tunapotumikia katika tengenezo la Yehova, twapaswa kuridhika kutumikia popote anapotugawia, na kufanya kazi tuliyopewa kwa uaminifu.
Toa neno au fungu la maneno yanayohitajiwa kukamilisha kila moja ya taarifa zifuatazo:
19. Ili kujionea kikamili hata zaidi baraka za Yehova, lazima twendelee kujifunza Biblia kwa ukawaida na kutoa ombi la bidii kwa Yehova atusaidie kuelewa na kutumia mafundisho ya Neno lake lililopuliziwa. (1 Tim. 4:8, 9) [1, w98-SW 1/1 uku. 24 fu. 6]
20. Kurairai humchukiza Yehova sana kwa sababu kunachochewa na ubinafsi, wala si kwa moyo mweupe wala ufuatiaji-haki, na zaidi ya yote, si kwenye upendo. [5, w98-SW 2/1 uku. 30 fu. 2-3]
21. Jina Yoshua humaanisha “Yehova Ni Wokovu,” naye alikuwa mfanani wa kiunabii wa Yesu. [9, si-SW uku. 42 fu. 5]
22. Kupatana na kielezi cha Yesu kwenye Mathayo 7:24-27, wazazi wenye busara wanaweza kusaidia watoto wao washinde mikazo iliyo kama dhoruba kwa kuwapa ujuzi sahihi na uelewevu utakaowasaidia kuendelea kuwa imara. [10, w98-SW 2/15 uku. 9 fu. 1]
23. Rekodi ya kihistoria iliyoandikwa katika kitabu cha Waamuzi huanzia kipindi cha wakati wa kifo cha Yoshua hadi wakati wa Samweli, yahusisha miaka kama 330. [15, si-SW uku. 47 fu. 5]
Chagua jibu sahihi katika kila moja ya taarifa zifuatazo:
24. Kuchukua hatua kuhusiana na matumizi ya mali yako iwapo kifo kingetokea ni (jambo la kutaniko; jambo la kibinafsi; takwa la Wakristo wa kweli). (Gal. 6:5) [3, w98-SW 1/15 uku. 19 fu. 6]
25. Paulo alimtia moyo Filemoni ampokee (Onamu; Onesiforo; Onesimo) kwa fadhili lakini hakutumia mamlaka ya kimitume kumwamuru afanye hivyo au kumweka huru mtumwa wake. (Flm. 21) [4, w98-SW 1/15 uku. 31 fu. 1]
26. Kupungukiwa kwenye uzito kunakomaanishwa katika simulizi la wakoma ambao waliponywa na Yesu ni (kukosa kwao imani; kutotii; kukosa shukrani). (Luka 17:11-19) [7, w98-SW 2/15 uku. 5 fu. 2]
27. Kwa kuwa Mungu alikubali mwendo wa Rahabu, maneno yake kwa wanaume wa Yeriko ambao walikuwa wakiwatafuta wapelelezi Waisraeli yaonyesha kwamba (kudanganya ni uamuzi wa mtu binafsi; mtu hana wajibu wa kutoa habari ya kweli kwa watu ambao hawana haki ya kuipokea; hakuwa amebadili njia zake za kilimwengu.) (Yos. 2:3-5; linganisha Waroma 14:4.) [9, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w93-SW 12/15 uku. 25 fu. 1.]
28. Kama ilivyorekodiwa kwenye Yohana 13:5, somo linalofundishwa kwa vielezo ambalo Yesu alifundisha hukazia sifa ya (fadhili; hisia-mwenzi; unyenyekevu), ambayo humfanya mtu awe tayari kufanya kazi za hali ya chini zaidi kwa niaba ya wengine. [13, w98-SW 3/15 uku. 7 fu. 6]
Patanisha maandiko yafuatayo na taarifa zilizoorodheshwa chini:
Kum. 7:3, 4; 17:7; 25:11, 12; 28:3; Yer. 15:20
29. Kwa kuwa Muumba huheshimu sana viungo vya uzazi jambo hilo lapasa kuathiri uamuzi ambao Mkristo hufanya kuhusu njia ifaayo ya kupanga uzazi. [Kum. 25:11, 12] [6, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w99-SW 6/15 uku. 28 fu. 2-5.]
30. Twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atatutegemeza tutimizapo utume wetu wa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. [Yer. 15:20] [12, w98-SW 3/1 uku. 27 fu. 6]
31. Kutii onyo la Biblia hutuepusha na matokeo yenye kuhuzunisha ambayo mara nyingi hutokea wakati Mkristo hujitia nira pamoja na mtu asiyeamini. [Kum. 7:3, 4] [2, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w89-SW 11/1 uku. 20 fu. 11.]
32. Kufurahia baraka za Mungu hakutegemei pale ambapo huenda tukawatunaishi au kutumikia au mgawo wowote ambao huenda tukawa nao katika utumishi wa Mungu. [Kum. 28:3] [7, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w96-SW 6/15 uku. 15 fu. 15.]
33. Mamlaka anayonukuu kwa maagizo yake katika 1 Wakorintho sura ya 5 juu ya kutengwa na ushirika, Paulo ananukuu Sheria ya Yehova. [Kum. 17:7] [4, Usomaji wa Biblia kila juma; ona si-SW uku. 213 fu. 24.]