Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/00 uku. 1
  • “Fulizeni Kuwa Macho”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Fulizeni Kuwa Macho”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • “Fulizeni Kulinda”!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Endelea Kukesha Katika “Wakati wa Mwisho”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Wenye Furaha ni Wale Wakaao Macho!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Dumisha Hisi Yako ya Uharaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 5/00 uku. 1

“Fulizeni Kuwa Macho”

1 Baada ya kusimulia matukio muhimu ambayo yangeashiria siku za mwisho za huu mfumo wa mambo, Yesu aliwasihi sana wanafunzi wake ‘wafulize kuwa macho.’ (Mr. 13:33) Kwa nini ni lazima Wakristo wafulize kuwa macho? Kwa sababu tunaishi nyakati zenye hatari zaidi katika historia ya binadamu. Lazima tuepuke hatari ya kusinzia kiroho. Tusipofanya hivyo tutakosa kuthamini kazi ambayo Yehova ametupa tufanye wakati huu wa mwisho. Kazi hiyo ni gani?

2 Yehova anawaamuru watu wake watangaze habari njema kuhusu Ufalme wake duniani kote—tumaini pekee kwa wanadamu. Kufanya kazi kwa ukaribu pamoja na tengenezo la Mungu hututambulisha kuwa Wakristo wa kweli wanaojali nyakati tunamoishi na wanaoona uhitaji wa kusaidia wengine wasikie “semi za uhai udumuo milele.” (Yn. 6:68) Kwa kushiriki kwa bidii kazi hii iliyo ya maana zaidi, twathibitisha kuwa tuko macho kiroho.

3 Twachochewa Kuhubiri: Tukiwa Mashahidi wa Yehova, twapaswa kuwa na maoni yanayofaa kuhusu huduma yetu. Kumpenda Mungu na jirani hutuchochea kibinafsi kuhubiri. (1 Kor. 9:16, 17) Kufanya hivyo, kutatuokoa na vilevile wale watusikilizao. (1 Tim. 4:16) Acheni tuazimie kuhubiri kwa ukawaida iwezekanavyo na kwa muda mrefu ihitajikavyo juu ya serikali iliyo bora zaidi ambayo wanadamu wanaweza kupata, yaani, Ufalme wa Mungu!

4 Twachochewa kufanya huduma yetu kwa hima na jambo fulani muhimu. Dhiki kubwa itafyatuka tunapoendelea na kazi hii. Kwa kuwa hatujui siku na saa twahitaji kufuliza kuwa macho na tayari wakati wote, huku tukimtegemea Yehova kwa sala. (Efe. 6:18) Eneo la kuhubiri linazidi kupanuka. Lakini siku moja hivi karibuni, kazi kubwa kupita zote ya kutoa ushahidi katika historia ya binadamu itafikia upeo.

5 Tii kwa uaminifu amri ya Yesu ya ‘kufuliza kuwa macho.’ Uhitaji huo ni muhimu zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote. Na tuitikie kwa hima. Acheni tuendelee kuwa makini kiroho, chonjo, na watendaji katika utumishi wa Yehova, leo na kila siku. Naam, na “tukae macho na kutunza hisi zetu.”—1 The. 5:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki