“Fulizeni Kuwa Macho”
1 Baada ya kusimulia matukio muhimu ambayo yangeashiria siku za mwisho za huu mfumo wa mambo, Yesu aliwasihi sana wanafunzi wake ‘wafulize kuwa macho.’ (Mr. 13:33) Kwa nini ni lazima Wakristo wafulize kuwa macho? Kwa sababu tunaishi nyakati zenye hatari zaidi katika historia ya binadamu. Lazima tuepuke hatari ya kusinzia kiroho. Tusipofanya hivyo tutakosa kuthamini kazi ambayo Yehova ametupa tufanye wakati huu wa mwisho. Kazi hiyo ni gani?
2 Yehova anawaamuru watu wake watangaze habari njema kuhusu Ufalme wake duniani kote—tumaini pekee kwa wanadamu. Kufanya kazi kwa ukaribu pamoja na tengenezo la Mungu hututambulisha kuwa Wakristo wa kweli wanaojali nyakati tunamoishi na wanaoona uhitaji wa kusaidia wengine wasikie “semi za uhai udumuo milele.” (Yn. 6:68) Kwa kushiriki kwa bidii kazi hii iliyo ya maana zaidi, twathibitisha kuwa tuko macho kiroho.
3 Twachochewa Kuhubiri: Tukiwa Mashahidi wa Yehova, twapaswa kuwa na maoni yanayofaa kuhusu huduma yetu. Kumpenda Mungu na jirani hutuchochea kibinafsi kuhubiri. (1 Kor. 9:16, 17) Kufanya hivyo, kutatuokoa na vilevile wale watusikilizao. (1 Tim. 4:16) Acheni tuazimie kuhubiri kwa ukawaida iwezekanavyo na kwa muda mrefu ihitajikavyo juu ya serikali iliyo bora zaidi ambayo wanadamu wanaweza kupata, yaani, Ufalme wa Mungu!
4 Twachochewa kufanya huduma yetu kwa hima na jambo fulani muhimu. Dhiki kubwa itafyatuka tunapoendelea na kazi hii. Kwa kuwa hatujui siku na saa twahitaji kufuliza kuwa macho na tayari wakati wote, huku tukimtegemea Yehova kwa sala. (Efe. 6:18) Eneo la kuhubiri linazidi kupanuka. Lakini siku moja hivi karibuni, kazi kubwa kupita zote ya kutoa ushahidi katika historia ya binadamu itafikia upeo.
5 Tii kwa uaminifu amri ya Yesu ya ‘kufuliza kuwa macho.’ Uhitaji huo ni muhimu zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote. Na tuitikie kwa hima. Acheni tuendelee kuwa makini kiroho, chonjo, na watendaji katika utumishi wa Yehova, leo na kila siku. Naam, na “tukae macho na kutunza hisi zetu.”—1 The. 5:6.