Pendeleo kwa Walio Wachanga
1 Wengi ambao sasa ni wazazi hukumbuka kwa furaha pendeleo walilofurahia walipokuwa watoto wakikua katika kweli—Siku ya Magazeti. Kazi hiyo ilianzishwa katika makutaniko yote mwaka wa 1949. Kila mtu alipaswa kukazia fikira kugawanya magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! siku moja katika juma barabarani, nyumba hadi nyumba, duka hadi duka, na katika njia nyingine. Wahubiri wachanga hasa walitazamia kwa hamu kushiriki kazi hii kwa sababu iliwapa fursa ya kushiriki utendaji uleule kama watu wazima kutanikoni. Je, ilikuwa hivyo ulipokuwa mtoto?
2 Husisha Watoto Wako: Watoto wachanga sana ambao hawako tayari kuanzisha mazungumzo ya Kimaandiko mlangoni bado wanaweza kutoa magazeti. Kufanya hivyo hutaka tu kujifunza utoaji sahili wa sentensi chache fupi. Labda maelezo mafupi kuhusu picha iliyo kwenye jalada yanaweza kutosha. Wenye nyumba wengi hukubali kwa utayari majarida kutoka kwa vijana wetu, mara nyingi wakisema vema kuhusu weupe wa moyo na mwenendo mzuri wa vijana hao. Watoto wanaweza kufanya utumishi huo vizuri zaidi na kuchangia ifaavyo kueneza ujumbe wa Ufalme wanaposaidiwa kidogo. Bila shaka, kadiri watoto wakuavyo, wazazi wao watataka kuwasaidia wazidi kufanya maendeleo katika kusitawisha ustadi wao wa kutoa ushahidi.
3 Manuel alianza kuhubiri mlango hadi mlango alipokuwa na umri wa miaka mitatu. Wazazi wake walimfundisha kukariri utoaji mfupi. Yeye huhubiri kwa bidii pamoja nao, akiangusha magazeti mengi, broshua, na trakti. Pia yeye hutoa ushahidi wa kivivi hivi. Katika pindi moja wazazi wake walipompeleka kwenye bustani kwa ajili ya tafrija, aliwafikia watu fulani waliokuwa hapo na kuwaangushia trakti kadhaa. Ijapokuwa angali mchanga sana, shauku ya Manuel kuelekea huduma ni kichocheo halisi kwa wazazi wake na kutaniko lote.—Mit. 22:6.
4 Kila Jumamosi imechaguliwa kuwa “Siku ya Magazeti” kwenye 2000 Calendar of Jehovah’s Witnesses. Wazazi, twapendekeza mwonyeshe upendezi mpya kuelekea kazi hii, mkiwasaidia watoto wenu wachanga washiriki kwa ukawaida kadiri iwezekanavyo katika pendeleo hili la utumishi.