Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/88 uku. 8
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Watoto

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Watoto
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WAKATI MCHANGA ANAPOFUNGUA MLANGO
  • Kuwalea Watoto Wako Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Wazazi—Zoezeni Watoto Wenu Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vijana—Fanyeni Moyo wa Yehova Ushangilie
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 11/88 uku. 8

Kutangaza Habari Njema—Kwa Watoto

1 Ukitazama huku na huku kwenye mikutano ya kundi iliyo mingi na hakika kwenye mikusanyiko mikubwa utaona ithibati kubwa kwamba kuna kikundi kikubwa cha ‘waume wachanga, mabikira, na wavulana’—ndiyo, watoto—wakisifu Yehova. (Zab. 148:12, NW) Jambo hili lapasa kukumbusha kila mmoja wetu uhitaji wa kuwapa wachanga tunaokuta katika utumishi wa shambani kila fursa ya kujifunza juu ya Yehova na ahadi zake. Kuwa kwetu chonjo na kujitayarisha kutolea watoto ushuhuda kutawapa fursa hii. Kuna mambo kadhaa ya uhakika yanayopasa kufikiriwa.

2 Kuwa na mwelekeo chanya kuhusu watoto na uwezo wao wa kukuza upendo kwa Yehova kunahitajiwa. Vielelezo vya Biblia, kama vile Samweli, Daudi, na Timotheo, vinaandaa uhakikisho wa kwamba walio wachanga katika umri wanaweza kujitoa kwa Mungu bila kukengeuka. (1 Sam. 2:18; Zab. 71:17; 2 Tim. 3:14, 15) Pia kuna vielelezo vya ki-siku-hizi.

WAKATI MCHANGA ANAPOFUNGUA MLANGO

3 Wakati mchanga anapofungua mlango, je! kama desturi wewe unaomba uzungumze na wazazi? Ikiwa wazazi hawapo je! wewe unaendelea kwenda kwenye mlango unaofuata? Uhai wa mchanga huyo ni wenye thamani pia. Mbona usirekebishe utoaji wako na ushiriki habari njema pamoja naye? Utoaji rahisi wenye kueleza Paradiso itakuwa ya namna gani au maneno mafupi kuhusu wakati ujao yanaweza kutumiwa kuamsha kupendezwa. Mathalani, watoto wengi wanafahamiana na sala ya Bwana na upesi wanaweza kuelewa maelezo yanayohusu kile ambacho jibu la sala hiyo litamaanisha kwa habari ya hali za ulimwengu zilizobadilika.

4 Katika kuwatolea watoto ushuhuda, ni jambo la maana kuheshimu mamlaka ya wazazi. Busara inapasa kutumiwa wakati wa kuwatolea watoto fasihi. Ikitegemea umri wao, lingekuwa jambo linalofaa kuwauliza ikiwa wazazi wao wanawaruhusu wachague habari zao wenyewe za kusoma. Ikiwa hawana ruhusa ya kukubali fasihi lakini wanaonyesha kupendezwa, watolee ushuhuda kwa mazungumzo kisha upange kuwarudia wazazi wao wakiwa nyumbani. Huenda hiyo ikawa jiwe la kukanyagia katika kuwasaidia wazazi pia.

5 Kuwa wenye kubadilika na walio chonjo kunatia ndani kutambua ya kwamba kuna kile ambacho wachanga wanahitaji. Tengenezo la Yehova limetayarisha vichapo vyenye kuvutia vyenye habari zinazoufaa wakati na ambazo zimetayarishwa kufikia wachanga wa umri zote. Mwalimu Mkuu na Hadithi za Biblia vinapendeza sana walio wachanga katika umri. Vitabu vya Ujana Wako na Maisha ya Jamaa vina habari hususa za kusaidia wale walio wakubwa zaidi katika umri. Na lo! ni hazina iliyoje inayopatikana katika magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Sehemu ya Amkeni! “Vijana Wanauliza . . . ” na mfululizo wa Mnara wa Mlinzi wa “Huduma na Maisha ya Yesu” ingefaa kwa kuwatolea watoto. Picha zenye rangi nne ambazo zimo katika magazeti yote hayo zinaweza kuchochea mawazo ya vijana na kuamsha ndani yao tamaa ya kujua Mungu ambaye ana daraka la uumbaji wa ajabu usio na kikomo. Jambo ambalo halipasi kusahauliwa ni broshua zenye rangi nzuri, kama vile Furahia Maisha Milele Duniani! Kwa hiyo unapojitayarisha kwa ajili ya utumishi wa shambani, fikiria kile ambacho unaweza kuchukua kinachoweza kuvutia wachanga.

6 Kutekelezwa kwa hukumu ya Yehova kutaathiri wote, kutia ndani “kijana, na msichana, na watoto wachanga.” (Eze. 9:6) Uhakika wa kwamba baadhi ya wale ambao wametumikia Yehova kwa miaka mingi walikubali ukweli wakiwa na umri mchanga unapasa utusaidie tuone uhitaji wa kuwatolea ushuhuda watoto tunaokuta katika huduma. Tunaweza kuonyesha hangaikio lenye upendo kama Yesu alivyofanya na kuleta baraka kwa kushiriki habari njema pamoja nao. (Mt. 19:14, 15) Uwe na mwelekeo chanya na uwatolee wachanga ushuhuda unaowafaa, ukiwa na tumaini la kwamba huenda wao pia wakawa wasifaji wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki