Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa miezi ya mikusanyiko. Makutaniko yaweza kufanya marekebisho yahitajiwayo ili kuruhusu uhudhuriaji wa Mkusanyiko wa Wilaya wa “Watekelezaji wa Neno la Mungu.” Inapofaa, tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa mwisho kabla ya kuhudhuria mkusanyiko ili kupitia shauri lililoonyeshwa katika nyongeza ya mwezi huu. Tieni moyo kila mmoja achukue dakika chache kuangalia programu iliyochapishwa kabla ya kipindi cha kila asubuhi na alasiri kuanza na kutazamia kwa hamu mambo yatakayozungumziwa. Hilo litafanya iwe rahisi zaidi kukazia fikira programu na kuandika mambo machache muhimu. Majuma mawili hadi manne baada ya mkusanyiko, pitio la mambo makuu ya programu la dakika 30 lapasa kupangwa kwenye Mkutano wa Utumishi. Wakati huo, kila mmoja atakuwa amejitayarisha kutoa maelezo mafupi anapoalikwa kufanya hivyo na ndugu watatu wanaostahili ambao walipewa mgawo mapema wa kushughulikia sehemu hii. Maelezo yaweza kuonyesha jinsi mambo tuliyojifunza mkusanyikoni yawezavyo kutumiwa kutanikoni na shambani. Jambo moja lililoonwa au mawili mafupi yaweza kusimuliwa. Sehemu hii ya Mkutano wa Utumishi yaweza kufanywa ipendeze na iwe yenye kufundisha ikiwa watu wote watajitayarisha vizuri.
Juma Linaloanza Mei 8
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Mzee atapitia kwa makini taarifa iliyo juu kuhusu marekebisho katika Mkutano wa Utumishi. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Je, Wewe Huthamini Mambo Matakatifu?” Hotuba itolewe na mzee. Kazia umuhimu wa kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko wa wilaya.
Dak. 15: “Acheni Mambo Yenu Yote Yatendeke kwa Upendo.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Simulia matatizo fulani yanayotokea watu wanapokosa kufuata mwelekezo uliotolewa wa kupata mahali pa kulala.
Wimbo 201 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 15
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 16: “Zingatia Matamko Yaliyo Matakatifu.” Maswali na majibu. Kazia sababu zinazopaswa kutufanya sisi sote tuwe tumeketi kila kipindi kinapoanza.
Dak. 16: “Dumisha Mwenendo Mzuri Unaomtukuza Mungu.” Mzee azungumzia makala pamoja na familia. Wazungumzia mambo wanayohitaji kufanya ili kudumisha utaratibu, tabia nzuri, usafi, na kielelezo katika sura na mwenendo mbele za umma wanapohudhuria mkusanyiko.
Wimbo 203 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 22
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Toa wonyesho uliotayarishwa vizuri juu ya kutoa kitabu Ujuzi katika mpango wa mchango kwenye mahubiri ya nyumba hadi nyumba. Mwenye nyumba auliza kitabu Ujuzi kinagharimu nini? Aambiwa kwamba tunaachia wale wanaopendezwa kukisoma bila kutoza gharama yoyote. Kisha mwenye nyumba aelezwa juu ya mpango wa kutoa mchango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. Ajitolea kutoa mchango wake naye mhubiri amshikia bahasha ili atie ndani mchango wake. Zungumzia Sanduku la Swali.
Dak. 20: “Fulizeni Kuwa Macho.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Eleza kwa nini ni jambo la hima kukaa macho kiroho hata ingawa hatujui siku na saa.—Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 1995, ukurasa wa 20.
Dak. 13: Unapangia Nini Agosti na Septemba? Familia yazungumzia kile watakachofanya Agosti na Septemba. Waongea juu ya kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko wa wilaya na kufanya upainia msaidizi mwezi mmoja au zaidi. Pia huenda kukawa na fursa ya kuzuru bustani yenye kuvutia au kujihusisha na tafrija inayofaa. Wote wakubali kutopuuza ratiba yao ya utendaji wa kitheokrasi.
Wimbo 83 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 29
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Mei. Toa onyesho fupi kuhusu toleo la kichapo la Juni. Onyesha jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia, ukitumia somo la 13 katika broshua Anataka.
Dak. 15: “Kupata Shangwe Katika Utumishi Wako Mtakatifu.” Hotuba. Zungumzia sababu zinazochangia shangwe katika huduma yetu. — Ona Insight, Buku la 2, ukurasa wa 120.
Dak. 18: Usomaji wa Biblia Unaothawabisha. Hotuba na maonyesho ikitegemea kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 34-35, fungu la 6-7. Mambo makuu ya Biblia ambayo hutegemea programu ya kiwango fulani ya usomaji wa Biblia, ni sehemu ya utaratibu wa masomo katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. (Huduma ya Ufalme Yetu, Desemba 1999, ukurasa wa 7) Panga familia itoe onyesho kuhusu jinsi ambavyo familia ingeweza kuchunguza sehemu ya juma hili ya usomaji wa shule. Wachagua jambo moja au mawili yenye kupendeza na kufanya utafiti zaidi katika Watch Tower Publications Index au Insight on the Scriptures. Onyesha jinsi usomaji wa Biblia uwezavyo kuwa wenye maana, ukituandaa ifaavyo ‘kulitumia sawasawa neno la ile kweli.’—2 Tim. 2:15.
Wimbo 95 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 5
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 15: “Pendeleo kwa Walio Wachanga.” Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Simulia jambo lililoonwa katika Mnara wa Mlinzi, Desemba 1, 1996, ukurasa wa 13, fungu la 15. Alika vijana wajikumbushe jinsi walivyofurahia kugawanya magazeti. Panga kijana mmoja au wawili watoe wonyesho wa utoaji sahili wa magazeti mlango hadi mlango. Watie moyo wazazi waambatane na watoto wao katika kazi ya magazeti kila juma.
Dak. 15: “‘Wajaribiwe Juu ya Kufaa’—Jinsi Gani?” Hotuba itolewe na mzee. Pitia mpango wa Kimaandiko wa kuwa na watumishi wa huduma katika kutaniko. (Ona Insight, Buku la 2, ukurasa wa 409.) Onyesha ni sifa zipi wanazohitaji kutimiza ili kuwekwa rasmi. (Ona kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 55-57.) Taja njia mbalimbali ambazo watumishi wa huduma hutumiwa, na kuwatia moyo akina ndugu zaidi wajitahidi kufikia pendeleo hilo.
Wimbo 82 na sala ya kumalizia.