Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Mei: Nakala mojamoja za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Uwe na broshua Anataka karibu kwa ajili ya watu wenye kupendezwa, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini? Kazia kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Julai na Agosti: Broshua zozote zifuatazo zenye kurasa 32 zaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? na Serikali Itakayoleta Paradiso. Broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kutusaidia au Kutuumiza? Je, Ziko Kweli?, na Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? zaweza kutolewa mahali panapozifaa. Pia vijitabu Habari Njema Hizi za Ufalme na Roho Zisizoonekana vyaweza kutumiwa miezi hii.
◼ Twaona uhitaji wa kuwakumbusha wahubiri wote kwamba anwani ya Sosaiti haipasi kutumiwa kamwe kwa barua zozote za kibinafsi. Hiyo yatia ndani barua zote na vichapo vinavyotumwa kwa wenye kupendezwa, wasiokuwako nyumbani, au kutolea ushahidi wale wanaoishi mahali pasipofikika. Unapotoa ushahidi kupitia barua, tumia ama anwani yako ya kibinafsi ama anwani ya Jumba la Ufalme. Tafadhali usitumie anwani ya Sosaiti.
◼ Tuna kaseti nyingi za drama, Doing God’s Will With Zeal katika Kiingereza. Makutaniko yanatiwa moyo kuagiza kaseti hiyo ili wahubiri wanufaike kwa kusikiliza drama hiyo.
◼ Mikusanyiko ya wilaya mitatu iliyofupishwa imepangwa Tanzania mwaka huu kama ionyeshwavyo:
Kigoma Agosti 26-27, 2000
Songea Agosti 26-27, 2000
Sumbawanga Agosti 5-6, 2000