Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 8
  • Mikutano Hunufaisha Vijana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Hunufaisha Vijana
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Jinsi ya Kupata Shangwe Zaidi Kutokana na Mikutano
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Jinsi Yehova Anavyotuongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 8

Mikutano Hunufaisha Vijana

1 Msichana mmoja tineja alisema hivi: “Nyakati fulani mimi hufikiri vijana ndio wenye wakati mgumu zaidi maishani. Sisi huwa tumezungukwa na watu wanaofanya uasherati, wanaotumia dawa za kulevya, na kunywa.” Je, ndivyo unavyohisi? Ikiwa ndivyo, je, wafikiri ni nini kitakachokusaidia kushinda uvutano huo mbaya? Wahitaji imani, imani yenye nguvu katika njia za Yehova za uadilifu, kwa kuwa bila hiyo “haiwezekani kumpendeza vema.” (Ebr. 11:6) Kuhudhuria mikutano ya kutaniko kutakusaidia kuimarisha usadikisho wako wa Kikristo na azimio lako la kuepuka lililo baya.

2 Mikutano Ina Mengi ya Kukupatia: Ni nini ambacho hufanya mlo mtamu pamoja na rafiki zako ufurahishe? Je, si mchanganyiko wa chakula kinachopendeza na ushirika wenye kupendeza katika mazingira yenye kustarehesha? Mikutano yetu hutoa hali kama hiyo yenye kupendeza, lakini katika namna ya kiroho.

3 Mambo yanayozungumziwa kwenye mikutano ni yenye kujenga, kuanzia mambo yanayoshughulika na matatizo ya kila siku ya maisha hadi mafunzo ya unabii wa Biblia wenye kusisimua. Maagizo yenye kutumika hutolewa ambayo hukufundisha jinsi ya kuishi njia bora zaidi ya maisha na kukabiliana na magumu unayoyapata. Waandamani unaowapata mikutanoni ni wazuri zaidi, na hali ya kiroho ni yenye kupendeza na salama. (Zab. 133:1) Si ajabu kijana mmoja alisema hivi: “Naenda shuleni mchana kutwa, nami huchoka. Lakini mikutano ni kama maji jangwani, ambapo naburudishwa ili kuweza kukabiliana na siku ifuatayo ya shule.” Mwingine alisema: “Nimeona kwamba kushirikiana kwa karibu pamoja na wengine wanaompenda Yehova hunisaidia niwe na uhusiano wa karibu naye.”

4 Kwa kujiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, wajifunza kukusanya habari ya Biblia, kuitayarisha iwe hotuba, kisha kuitoa kwa njia ya mazungumzo mbele ya wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Hebu wazia manufaa ya kuzoezwa kufundisha kweli zenye kuokoa uhai za Neno la Mungu kwa ustadi! Ni wapi kwingine ambako vijana wanaweza kupata mazoezi yenye thamani kama hayo?

5 Jinsi ya Kupata Faida Kutokana na Mikutano: Ili unufaike na mikutano, kuna mambo matatu ya muhimu yanayohusika. Hayo ni kutayarisha, kushiriki, na kutumia unayojifunza.

6 Jitayarishe kwa Ajili ya Mikutano: Weka ratiba ya wakati ya kujitayarisha kwa ajili ya mikutano kwa ukawaida. Usiruhusu kazi ya shuleni, kazi ya muda, au tafrija zifanye ukose wakati unaohitaji wa kutayarisha mapema habari itakayozungumziwa kwenye kila mkutano. Kuwa na utaratibu mzuri kutasaidia. Kwanza kabisa, endelea kufuatana na usomaji wa Biblia wa kila juma ulioratibiwa wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Huchukua dakika chache tu kila siku kusoma na kutafakari sura ulizogawiwa. Weka kando wakati utayarishe Funzo la Kitabu la Kutaniko na Funzo la Mnara wa Mlinzi. Wengine hufanya hivyo siku moja au mbili hivi kabla ya mikutano hiyo. Ikiwezekana, fanya vivyo hivyo kwa sehemu za Mkutano wa Utumishi kila juma.

7 Shiriki Katika Mikutano: Biblia husema kwamba akiwa na umri wa miaka 12, Yesu alipatikana hekaluni, akisikiliza, akiuliza maswali, na kutoa majibu. (Luka 2:46, 47) Yaani, alishiriki kabisa. Utanufaika zaidi kutokana na mikutano unapojitahidi kuishiriki.—Mit. 15:23.

8 Unahitaji kuwa makini kwa yale yanayofundishwa mikutanoni. Nyakati nyingine, ni vigumu kusikiliza hotuba kuliko kuitoa. Kwa nini? Huenda akili yako ikatangatanga mtu fulani anapoongea. Unaweza kushindaje jambo hilo? Kwa kuandika. Andika mambo ya maana unayotaka kuyarejezea baadaye. Kuandika kutakusaidia kukaza akili yako kwenye programu. Pia, fungua maandiko, na ufuatane na msemaji anapoyasoma.

9 Kwa kuongezea, weka mradi wa kushiriki katika kila sehemu ya mazungumzo ya maswali na majibu kwenye mikutano. Utanufaika hata zaidi ukitafakari yale unayotaka kusema. Mithali 15:28 husema: “Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu.”

10 Tumia Yale Unayojifunza: Hatua ya mwisho ni kuhakikisha kwamba yale unayojifunza ‘yafanya kazi katika wewe.’ (1 The. 2:13) Unapotumia mambo mazuri uliyojifunza mkutanoni, utakuwa na uhusiano wa karibu zaidi na Yehova Mungu. Atakuwa halisi kwako, nawe utakuwa na shangwe na uradhi mwingi ‘unapoendelea kutembea katika kweli,’ ukiifanya iwe yako mwenyewe.—3 Yoh. 4.

11 Ndugu na dada wachanga, mnapojitayarisha kwa ukawaida kwa ajili ya mikutano, kuishiriki, na kutumia yale mnayojifunza, mtafurahia mikutano kabisa. Wakati huohuo, mtapata faida zote mnazoweza kutokana nayo. Imani yenu, na vilevile azimio lenu la kudumu mkiwa waaminifu kwa Baba yenu wa kimbingu, Yehova litaimarishwa.—Zab. 145:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki