Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/00 uku. 1
  • Baraka ya Yehova Hututajirisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baraka ya Yehova Hututajirisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Hatujapata Kamwe Kuwa na Hali Nzuri Hivi ya Kiroho!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • ‘Tukiwa Hatuna Kitu Lakini Tukiwa na Vitu Vyote’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Je, Wewe Ni “Tajiri Kwa Mungu”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • ‘Tunda la Roho’ Linamtukuza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 9/00 uku. 1

Baraka ya Yehova Hututajirisha

1 Mara nyingi, mafanikio ya mtu hupimwa kwa mshahara wake. Ndiyo sababu watu wengi huona wale walio na pesa kuwa watu wenye furaha zaidi na wenye kuridhika zaidi. Hata hivyo, watu ambao huhisi kwamba pesa zaweza kununua furaha wamekosea sana. (Mhu. 5:12) Hakuna shangwe yenye kudumu kwa wale “waazimiao kuwa matajiri” kimwili. (1 Tim. 6:9) Kinyume cha hilo, watumishi wa Yehova wana shangwe kwelikweli na ni watu matajiri zaidi ulimwenguni. (Mit. 10:22; Ufu. 2:9) Jinsi gani?

2 Uthibitisho wa Utajiri Wetu: Sisi tuna ufahamu wa kiroho wenye kina na uelewevu wa Neno la Mungu, Biblia. Kupitia tengenezo lake la kidunia, Yehova huendelea kutufundisha juu yake mwenyewe na Mwanaye, ili tunufaike kabisa. Uelewevu sahihi hutuwezesha kuwa na uhusiano wa karibu zaidi na Yehova. (Yak. 4:8) Kutambua lililo jema na lililo baya na kufuata sheria za Mungu hutulinda na maradhi na hatari fulani-fulani. Tuna uhakika kwamba Yehova atatuandalia, tupate uradhi wa kimungu na amani ya akili.—Mt. 6:33.

3 Twafurahia amani na umoja miongoni mwa udugu wetu wa kiroho kwa sababu ya kusitawisha matunda ya roho ya Mungu. Tukiwa tumeunganishwa na kifungo chenye nguvu cha upendo, hatuhitaji kuhisi tumeachwa na Mungu au na ndugu zetu maafa yanapotupata.—Gal. 6:10.

4 Maisha yetu yana maana na kusudi halisi. Twaliona kuwa pendeleo kubwa ajabu kushiriki katika kuhubiri habari njema ulimwenguni pote. Hiyo hutuletea shangwe tunaposaidia watu wengine wawe na uhusiano mzuri pamoja na Mungu na kutumikia kwa umoja pamoja nasi katika ibada safi. Hazina yetu yenye thamani ya huduma humletea Yehova heshima na kutupa uradhi wa kuchangia kulitakasa jina lake. Twadumisha mtazamo ufaao wa akilini, tukijua kwamba tumaini letu la wakati ujao litatimizwa hivi karibuni.

5 Kuonyesha Uthamini Wetu: Sikuzote na tuthamini baraka za Yehova, ambazo hutufanya tuwe watu matajiri zaidi ulimwenguni. (Mit. 22:4) Kwa kutafakari kila siku yale tuliyo nayo sisi huchochewa kumshukuru Yehova kwa upendo wake mkarimu na kuendelea kumpa ujitoaji wetu usiohusisha mwingine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki