Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/00 uku. 1
  • Maisha Yamo Hatarini!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maisha Yamo Hatarini!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Endelea Kuhubiri!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kukunjuka Katika Upendo Wetu kwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 9/00 uku. 1

Maisha Yamo Hatarini!

1 Biblia hueleza wazi mapenzi ya Yehova “kwamba watu wa namna zote waokolewe.” Hata hivyo, ni kweli kwamba matazamio ya uhai ya mabilioni ya watu duniani hutegemea mtazamo wao kuelekea Yehova Mungu na Ufalme wake kupitia Yesu Kristo. Mtazamo unaofaa wategemea tu “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:3, 4) Huku tukitoa onyo kwamba hivi karibuni dunia itasafishwa iondolewe uovu wote ili ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu uwepo, pia tumeamuriwa kufanya kazi ya maana ya kuokoa uhai.—Mt. 24:14; 28:19, 20; Rom. 10:13-15.

2 Kwa Nini Ni ya Haraka Hivyo? Yesu alitoa onyo juu ya “dhiki kubwa ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu.” (Mt. 24:21) Dhiki hiyo kubwa itafikia upeo wake kwenye Har–Magedoni. (Ufu. 16:16) Watu wengi watakaoharibiwa wakikataa kukubali habari njema wanatia ndani watu wetu wa ukoo wasioamini, majirani, wafanyakazi wenzi, wanashule wenzi, na watu tunaowafahamu. Lakini hangaiko letu ni kufikia “watu wa namna zote” tukimwiga Mungu, ambaye alionyesha upendo wake kwa jamii nzima ya wanadamu kwa kumtoa Mwanaye, Yesu Kristo, awe fidia ya wote. (Yn. 3:16) Lazima tujitahidi kwa bidii kualika wote wakimbilie mahali pa Mungu penye usalama. Kwa kutimiza kazi ya kuhubiri kikamili, twaweza kuepuka hatia ya damu.—Eze. 33:1-7; 1 Kor. 9:16.

3 Lengo Letu Ni Nini? Umuhimu wa kazi ya kuhubiri wakaziwa kotekote katika Neno la Mungu. Kama ilivyoelezwa na mtume Paulo, “upendo alio nao Kristo hutushurutisha” kuishi kupatana na njia za Mungu. (2 Kor. 5:14) Kwa kuongezea, mara nyingi Mnara wa Mlinzi hukazia wajibu wetu wa kuhubiri. Huduma Yetu ya Ufalme huendelea kutuandalia mwongozo wa jinsi ya kufanya kazi ya kuhubiri. Wazee hupanga kazi hii nao hututia moyo tuishiriki. Wahubiri wenzetu hutualika twende nao katika huduma. Sisi husikia mengi kuhusu kutayarisha utoaji wetu mbalimbali, kutoa magazeti na vichapo vingine, kufanya ziara za kurudia, kuongoza mafunzo ya Biblia, na kutumia kila fursa kutoa ushahidi. Yote hayo hutusaidia tutimize lengo letu la kuokoa uhai.—1 Kor. 9:22, 23; Efe. 1:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki