Endelea Kuhubiri!
1 Ni mapenzi ya Mungu kwamba “watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Ndiyo sababu ametupa mgawo wa kuhubiri habari njema. (Mt. 24:14) Tukithamini sababu ya kuendelea kuhubiri, hatutazuiwa na chochote kitakachoelekea kutuvunja moyo au kutukengeusha fikira.
2 Kwa Nini Tuendelee? Kuna vikengeusha fikira vingi ulimwenguni ambavyo hufanya watu wasahau au wapuuze yale tunayowaambia. Kwa hiyo, lazima twendelee kuwakumbusha ujumbe wa Mungu wa wokovu. (Mt. 24:38, 39) Kwa kuongezea, hali za maisha ya watu zabadilika sikuzote. Hata hali za ulimwengu zaweza kubadilika kabisa mara moja. (1 Kor. 7:31) Kesho, juma lijalo, au mwezi ufuatao, watu ambao tunawahubiria huenda wakakabili matatizo au mahangaiko yatakayowafanya wafikirie kwa uzito zile habari njema tunazowapelekea. Je, hushukuru kwamba Shahidi aliyekuletea kweli aliendelea kuja?
3 Kuiga Rehema ya Mungu: Yehova ameruhusu kwa subira wakati upite kabla ya kutekeleza hukumu dhidi ya waovu. Kupitia sisi ameendelea kuvuta watu wenye mioyo minyoofu wamrudie ili kuokolewa. (2 Pet. 3:9) Tungekuwa na hatia ya damu kama hatungeendelea kuwapa watu ujumbe wa Mungu wa rehema na kuwaonya juu ya hukumu ya Mungu inayokuja kwa wote wasioacha njia zao mbaya. (Eze. 33:1-11) Hata ingawa si wote wanaosikiliza tunapohubiri, hatupaswi kulegea kamwe kujitahidi vilivyo kusaidia watu wenye mioyo minyoofu wathamini rehema kubwa ya Mungu.—Mdo. 20:26, 27; Rom. 12:11.
4 Kuonyesha Upendo Wetu: Ni Yehova Mungu kupitia Yesu Kristo, ambaye aliagiza habari njema ihubiriwe duniani kote. (Mt. 28:19, 20) Hata watu wakikataa kusikiliza, tuna fursa ya kuonyesha upendo na ujitoaji wetu kwa Mungu kwa kuendelea kufanya yaliyo sawa.—1 Yoh. 5:3.
5 Na tuazimie kuendelea kuhubiri! Na tufanye hivyo kwa bidii maadamu hii ingali ‘siku ya Yehova ya wokovu.’—2 Kor. 6:2.