“Neno Linenwalo Wakati wa Kufaa”
1 Je, kuwaambia wengine ujumbe wa uhai ni jambo gumu kwako? Je, unahisi kwamba lazima useme mambo yenye kina sana ili uwapendeze wasikilizaji wako? Yesu alipowatuma wanafunzi wake, aliwaambia hivi: “Mwendapo, hubirini, mkisema, ‘Ufalme wa mbingu umekaribia.’” (Mt. 10:7) Ujumbe huo haukuwa mgumu sana kuutoa. Ndivyo ulivyo leo.
2 Mara nyingi ni maneno machache tu yanayohitajiwa ili kuanzisha mazungumzo. Filipo alipokutana na towashi Mwethiopia, alimwuliza hivi: “Je, wewe kwa hakika wajua unayoyasoma?” (Mdo. 8:30) Kulikuwa na mazungumzo yenye matokeo kama nini yaliyotokana na “neno linenwalo wakati wa kufaa”!—Mit. 25:11.
3 Waweza kutumia mfikio kama huo katika huduma yako. Jinsi gani? Kwa kuwa mwenye utambuzi na kuchagua maneno yanayofaana na hali. Uliza swali, na usikilize jibu.
4 Baadhi ya Maswali Rahisi: Ili kuanzisha mazungumzo, unaweza kujaribu lolote kati ya maswali haya:
◼ “Je, wewe husali ile Sala ya Bwana (au Baba Yetu) katika ibada yako?” (Mt. 6:9, 10) Kariri sehemu fulani, na useme: “Watu wengine huuliza, ‘Jina la Mungu ambalo Yesu alisema litakaswe (au litukuzwe) ni gani?’ Wengine huuliza, ‘Ufalme ambao Yesu alisema tuombe uje ni gani?’ Je, umepata majibu yenye kuridhisha ya maswali haya?”
◼ “Je, umepata kujiuliza hivi: ‘Maana ya uhai ni nini?’” Onyesha kwamba yahusiana na ujuzi kuhusu Mungu.—Mhu. 12:13; Yn. 17:3.
◼ “Je, wafikiri kifo kitawahi kukomeshwa kabisa?” Tumia Isaya 25:8 na Ufunuo 21:4 kutoa jibu lifaalo.
◼ “Je, kuna utatuzi rahisi kwa msukosuko ulio ulimwenguni?” Onyesha kwamba Mungu hufundisha hivi, ‘mpende jirani yako.’—Mt. 22:39.
◼ “Je, msiba wa ulimwengu wote utaangamiza dunia yetu siku moja?” Mwonyeshe ahadi ya Biblia ya kwamba dunia itadumu milele.—Zab. 104:5.
5 Toa habari njema kwa njia sahili, ya moja kwa moja na kwa mfikio wenye fadhili. Yehova atabariki jitihada zako za kushiriki angalau “neno” la kweli na wengine.