Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 2
  • Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Filipo Alifanya Nini?
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Filipo?
  • Mwige Filipo
  • Filipo—Mweneza-Evanjeli Mwenye Bidii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuanzisha Mazungumzo ili Kutoa Ushahidi Isivyo Rasmi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kupendezwa na Watu
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 2

KUANZISHA MAZUNGUMZO

Filipo mweneza injili akizungumza na mwanamume Mwethiopia anayesoma kitabu cha kukunjwa akiwa ndani ya gari linalokokotwa na farasi.

Matendo 8:​30, 31

SOMO LA 2

Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida

Kanuni: “Neno linalosemwa wakati unaofaa —ni jema sana!”—Met. 15:23.

Filipo Alifanya Nini?

Filipo mweneza injili akizungumza na mwanamume Mwethiopia anayesoma kitabu cha kukunjwa akiwa ndani ya gari linalokokotwa na farasi.

VIDEO: Filipo Anamhubiria Towashi Mwethiopia

1. Tazama VIDEO, au soma Matendo 8:​30, 31. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Filipo alianzishaje mazungumzo?

  2. Kwa nini hiyo ilikuwa njia ya kawaida ya kuanzisha mazungumzo na kumfundisha mwanamume huyo jambo jipya?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Filipo?

2. Ikiwa tutazungumza kwa njia ya kawaida, huenda mtu huyo akahisi vizuri zaidi na akawa tayari kusikiliza ujumbe wetu.

Mwige Filipo

3. Uwe mwenye utambuzi. Unaweza kujua mambo mengi kumhusu mtu kwa kutazama ishara za uso na mwili wake. Je, mtu huyo anaonekana yuko tayari kuzungumza nawe? Unaweza kuanzisha mazungumzo kuhusu kweli ya Biblia kwa kusema, “Je, ulijua kwamba . . . ?” Usimlazimishe mtu ambaye hataki kuzungumza nawe.

4. Uwe na subira. Usihisi kwamba ni lazima uanze mara moja kwa kuzungumzia kweli ya Biblia. Subiri wakati unaofaa ili uzungumzie kweli hiyo kwa njia ya kawaida. Huenda hilo likamaanisha kusubiri mpaka wakati mwingine utakapozungumza tena na mtu huyo.

5. Badilika kulingana na hali. Huenda mtu akazungumza jambo ambalo hukutarajia. Hivyo, uwe tayari kuzungumzia habari itakayomfaa mtu huyo, hata ikiwa mtazungumzia kweli ya Biblia tofauti na ile uliyopanga.

SOMA PIA

Mhu. 3:​1, 7; 1 Kor. 9:22; 2 Kor. 2:17; Kol. 4:6

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki