Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuanzisha Mazungumzo ili Kutoa Ushahidi Isivyo Rasmi
Kwa Nini Ni Muhimu: Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, mara nyingi sisi hatuwapati watu wengi katika nyumba zao. Hata hivyo, tunaweza kukutana na watu hao tunapotumia usafiri wa umma, tunaposubiri kumwona daktari, tunapokuwa mapumziko kazini au shuleni, na mahali kwingineko. Ni mapenzi ya Yehova kwamba watu wote, wapate fursa ya kusikia ujumbe wa Ufalme. (1 Tim. 2:3, 4) Kwa kawaida, ili kutoa ushahidi, ni lazima tuchukue hatua ya kwanza kuanzisha mazungumzo.
Jaribu Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Kila juma jaribu kuanzisha mazungumzo angalau mara moja, kwa lengo la kutoa ushahidi isivyo rasmi.