Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 1
  • Kupendezwa na Watu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupendezwa na Watu
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alifanya Nini?
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
  • Mwige Yesu
  • Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuanzisha Mazungumzo Yatakayokusaidia Kutoa Ushahidi
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuanzisha Mazungumzo ili Kutoa Ushahidi Isivyo Rasmi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 1

KUANZISHA MAZUNGUMZO

Yesu akizungumza na mwanamke kisimani.

Yohana 4:​6-9

SOMO LA 1

Kupendezwa na Watu

Kanuni: “Upendo . . . hautafuti faida zake wenyewe.”—1 Kor. 13:​4, 5.

Yesu Alifanya Nini?

Yesu akizungumza na mwanamke kisimani.

VIDEO: Yesu Akiwa na Mwanamke Kisimani

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 4:​6-9. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Yesu aliona nini kabla ya kuanzisha mazungumzo?

  2. Yesu akamwambia: “Naomba maji ninywe.” Kwa nini hiyo ilikuwa njia bora ya kuanzisha mazungumzo?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunaweza kuwa na mazungumzo mazuri ikiwa tutaanza kuzungumzia habari inayompendeza mtu.

Mwige Yesu

3. Badilika kulingana na hali. Usilazimishe kuanzisha mazungumzo kutokana na habari uliyopanga kuzungumzia. Anzisha mazungumzo kuhusu mambo ambayo watu wanafikiria siku hiyo. Jiulize:

  1. ‘Taarifa za habari zinazungumzia nini?’

  2. ‘Majirani, wafanyakazi, au wanafunzi wenzangu wanazungumzia mambo gani?’

4. Uwe mwenye utambuzi. Jiulize:

  1. ‘Mtu huyu anafanya nini sasa? Huenda anafikiria mambo gani?’

  2. ‘Mavazi, mwonekano, au nyumba yake inaonyesha nini kuhusu mambo anayoamini au utamaduni wake?’

  3. ‘Je, huu ni wakati unaofaa kuzungumza naye?’

5. Sikiliza.

  1. Usizungumze kupita kiasi.

  2. Mtie moyo ashiriki mazungumzo. Ikiwa inafaa, muulize maswali.

SOMA PIA

Mt. 7:12; 1 Kor. 9:​20-23; Flp. 2:4; Yak. 1:19

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki