Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/00 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 13
  • Juma Linaloanza Novemba 20
  • Juma Linaloanza Novemba 27
  • Juma Linaloanza Desemba 4
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 11/00 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Novemba 13

Wimbo 4

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Eleza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma huu.

Dak. 13: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.

Dak. 22: “Kusitawisha Upendezi Uliochochewa na Trakti Habari za Ufalme Na. 36.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya fungu la 1-5. Eleza mipango ya kukamilisha eneo lolote ambalo bado halijahubiriwa. Zungumzieni utoaji mbalimbali uliotajwa kwenye fungu la 7 na la 8 kuhusu kufanya ziara za kurudia, na kuwe na onyesho kwenye kila moja ya utoaji huo. Kazia umuhimu wa kufuatia watu wowote waliopendezwa na kujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Malizia kwa kuzungumzia fungu la 9 na maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa.

Wimbo 63 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 20

Wimbo 111

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mambo Yaliyoonwa Kuhusu Kugawanya Trakti Habari za Ufalme Na. 36. Simulia mafanikio ya kukamilisha eneo. Je, kuna wowote katika kutaniko walioshiriki katika utumishi wa shambani kwa mara ya kwanza? Simulia maelezo yenye kupendeza yaliyotolewa na wenye nyumba. Je, wahubiri fulani waliweza kuanzisha mafunzo ya Biblia? Ikiwa ndivyo, waombe wasimulie jinsi walivyofanya hivyo. Wakumbushe wote wasitawishe upendezi uliopatikana.

Dak. 20: “Endelea Kuhubiri!” Hotuba na mahoji. Wengine wamekuwa wakishirikiana na tengenezo la Yehova na wameendelea kuhubiri maisha yao yote. Wakiwa na mtazamo unaofaa, wamepata shangwe katika kufanya hivyo. (Ona kitabu Ujuzi, ukurasa wa 179, fungu la 20, na Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1992, ukurasa wa 21-22, fungu la 14-15.) Alika mhubiri mmoja ambaye amekuwa mtendaji kwa miaka mingi asimulie sababu ambazo zimemfanya aendelee kuhubiri.

Wimbo 141 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 27

Wimbo 153

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Novemba. Toleo la vichapo la Desemba ni kitabu Ujuzi na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Eleza jinsi ambavyo Mashahidi wa Yehova wametimiza fungu kubwa katika kuchapisha Biblia katika lugha nyingi.—Ona Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1997, ukurasa wa 11-12.

Dak. 20: Tumia Vizuri Kitabu Kutoa Sababu. Mazungumzo ya maswali na majibu ya ukurasa wa 7-8. Onyesha jinsi kitabu hiki kimekusudiwa kutusaidia tujitayarishe kutoa ushahidi wenye matokeo zaidi katika huduma. Eleza jinsi kitabu hicho kinavyoweza kutumiwa kutoa ushahidi kwa kutumia simu. Toa onyesho la jinsi ya kupata habari muhimu ili kujibu swali fulani. Sihi wote wasome kitabu hicho vizuri, wakibebe kwenye mikoba yao ya mahubiri, na kukitumia kwa ukawaida.

Dak. 15: Naweza Kudhibitije Mazoea Yangu ya Kutazama Televisheni? Mzee azungumza na ndugu kijana ambaye hutumia muda wa saa nyingi kwa siku kutazama televisheni. Kwanza, ndugu huyo anasisitiza kwamba hakuna ubaya wa kuitazama. Anasema kwamba ni njia fulani ya kujitumbuiza tu na kwamba haimwathiri vibaya. Mzee azungumzia mambo makuu yaliyo katika sura ya 36 ya kitabu Vijana Huuliza. Anaeleza kwamba kutazama televisheni kupita kiasi humaliza wakati wenye maana ambao waweza kutumiwa kufanya funzo la kibinafsi, kwenda katika huduma, au kusaidia kutimiza mahitaji ya kutaniko. Ndugu mchanga aonyesha uthamini kwa shauri hilo na kusema kwamba ili anufaike kiroho, atabadili mazoea yake ya kutazama televisheni. Katika makutaniko ambamo kutazama televisheni si tatizo, chunguzeni mahitaji ya kwenu.

Wimbo 175 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 4

Wimbo 189

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. “Useme Nini Kwenye Mashine ya Kujibia Simu?”

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Neno Linenwalo Wakati wa Kufaa.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji na maonyesho. Wengi huhisi kwamba hawana uwezo wa kutosha wanapojaribu kuanzisha mazungumzo, wakiwazia kimakosa kwamba wanahitaji ustadi wa pekee ili kufanikiwa. Eleza jinsi sisi sote, kutia ndani wahubiri wapya na wachanga, tunavyoweza kuanzisha mazungumzo tukijitahidi kwa kiasi fulani. Zungumzia utoaji mbalimbali uliodokezwa, ukikazia usahili wake, na panga wahubiri wawili au watatu watoe maonyesho kuyahusu. Rejezea Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998, ukurasa wa 8, kwa utoaji mbalimbali wa ziada ambao waweza kutumiwa. Sihi wote wawe na mwelekeo unaofaa ili wapate shangwe zaidi katika huduma yao.

Wimbo 218 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki