Useme Nini Kwenye Mashine ya Kujibia Simu?
Simu ni chombo chenye matokeo katika kuhubiria watu ambao hawawezi kupatikana nyumbani au ambao wanaishi kwenye maeneo yasiyoingiwa kwa urahisi. Hata hivyo, watu wengi zaidi hawajibu simu—wao hutumia mashine ya kujibia simu. Ukipata hali hiyo unaweza kufanya nini? Usikate simu. Badala yake, panga maandishi yaliyotayarishwa vizuri unayoweza kusoma kwenye simu. Jizoeze kuyasoma kwa njia yenye kupendeza, kwa namna ya mazungumzo. Unaweza kusema nini?
Unaweza kutoa mwaliko mchangamfu kwa mwenye nyumba ahudhurie Mkutano wa Watu Wote unaofuata kwenye Jumba la Ufalme. Labda waweza kusema hivi: “Nasikitika kwamba sikukupata nyumbani. Kama ungependa kusikia mazungumzo ya Biblia yanayohusu [kichwa cha hotuba], tafadhali njoo kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Watu wote wanaalikwa. Hakuna kukusanya sadaka.” Kisha sema waziwazi siku na saa ya mkutano, na ueleze jina la barabara au ufafanue mahali Jumba la Ufalme lipo.
Uwe macho kuona watu wowote wanaohudhuria mikutano kwa mara ya kwanza, jijulishe kwao, na uwakaribishe. Usisahau kuwaalika wawe na funzo la Biblia la nyumbani bila malipo!