Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/09 uku. 2
  • Kuhubiri kwa Simu Kunaweza Kuwa na Matokeo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri kwa Simu Kunaweza Kuwa na Matokeo
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Mahubiri ya Simu Yenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kutoa Ushahidi kwa Simu —Njia ya Kufikia Wengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Mlangoni na Kupitia Simu Inapowezekana au Kupitia Barua
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kuwatafuta Wale Wanaostahili
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 10/09 uku. 2

Kuhubiri kwa Simu Kunaweza Kuwa na Matokeo

1. Kwa nini kuhubiri kwa simu kunaweza kuonwa kuwa sehemu muhimu ya huduma yetu?

1 Kwa nini huenda tukafikiria kuhubiri kwa simu? Kwa sababu hiyo ni njia nyingine ya kuwasaidia watu kupata ujuzi sahihi kwa ajili ya wokovu. (2 Pet. 3:9) Ingawa njia yetu kuu ya kutangaza habari njema za Ufalme wa Mungu ni kuhubiri nyumba kwa nyumba, tunakuwa tayari kutumia njia nyinginezo ili kuwafikia watu ambao huenda tusiwapate nyumbani.—Mt. 24:14; Luka 10:1-7; Ufu. 14:6.

2. Ni utaratibu gani tunaoweza kufuata tunapohubiri kwa simu?

2 Utaratibu wa Kufuata: Wahubiri wanaotumia simu kuhubiri wanaweza kugawiwa eneo kama inavyofanywa katika mpango wa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Wanaweza kuhubiri wakiwa mtu mmojammoja au wakiwa kikundi kidogo cha watu wawili au watatu. Wanapaswa pia kufanya hivyo wakiwa mahali patulivu, pasipo na kelele. Wengi huona inafaa kuketi mezani wakiwa na vifaa vyote ambavyo kwa kawaida wanatumia wanapohubiri nyumba kwa nyumba.

3. Tunapaswa kukumbuka mambo gani tunapohubiri kwa simu?

3 Jinsi ya Kuhubiri kwa Simu: Tunapotumia simu kuhubiri, tunapaswa kuongea na watu jinsi tunavyoongea katika hali za kawaida. Wale ambao hawana uzoefu wa kuhubiri kwa simu wanaweza kumsomea mwenye nyumba mambo ambayo wangependa kumweleza, lakini wayasome kana kwamba wanazungumza naye katika hali za kawaida. Tangulizi zinazopatikana katika kitabu Kutoa Sababu, Huduma Yetu ya Ufalme, na trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? zinaweza kuwasaidia wale wanaohubiri kwa simu. Unapotayarisha habari ya kuzungumzia na mwenye nyumba, chagua kichwa, swali utakalouliza, na uwe tayari kusoma maandiko kadhaa yanayojibu swali hilo. Kwa kawaida utamweleza kuhusu toleo linaloachiwa wenye nyumba pindi hiyo. Fikiria vikumbusho hivi: Tulia na uzungumze polepole. Uwe mwenye heshima, subira, na urafiki unapozungumza kwa simu, kwa kuwa mwenye nyumba anaweza kujua usipokuwa na sifa hizo. Msikilize mwenye nyumba anapotoa maoni yake, kisha umshukuru. Uwe mwangalifu usitaje mpango wa kutoa michango, kwa sababu anaweza kufikiri kimakosa kuwa hiyo ni mbinu ya kuomba pesa.

4. Kuhubiri kwa simu hutuwezesha kutimiza nini katika eneo tulilogawiwa?

4 Huenda mtu unayemhubiria kwa simu ni mlemavu, mgonjwa, au mtu ambaye ratiba yake ya kazi inafanya iwe vigumu kumpata unapohubiri nyumba kwa nyumba. Wengine wanaishi katika majengo ambayo watu wasioishi humo hawaruhusiwi kuingia. Kwa hiyo, tunapojitahidi kutimiza huduma yetu kwa ukamili, na tufikirie kutumia mbinu hii yenye matokeo ya kuhubiri kwa simu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki