Kuwatafuta Wale Wanaostahili
1 Huenda isiwe rahisi kufuata maagizo ya Yesu kuhusu kazi ya kuhubiri. Aliagiza hivi: “Katika jiji lolote lile au kijiji chochote kile mtakapoingia, tafuteni ni nani humo anayestahili.” (Mt. 10:11) Kwa kuwa si rahisi kuwapata watu nyumbani siku hizi, tunawezaje kuwatafuta na kuwapata wale wanaostahili?
2 Chunguza Eneo Lenu: Kwanza chunguza eneo lenu. Kwa kawaida, watu hupatikana nyumbani wakati gani? Wanaweza kupatikana wapi mchana? Je, kuna siku fulani au wakati fulani ambapo huenda wakatukaribisha na kutusikiliza? Unaweza kupata matokeo zaidi ukibadili ratiba yako ya kuhubiri ili iwafae watu katika eneo lenu.—1 Kor. 9:23, 26.
3 Wahubiri wengi wamefanikiwa kuwapata watu nyumbani saa za jioni. Baadhi yao huwa wamestarehe zaidi na huwa tayari kutusikiliza wakati huo. Tunaweza pia kuwafikia watu kwa kuhubiri habari njema katika maeneo ya kibiashara na sehemu za umma.
4 Katika mwezi mmoja wa utendaji wa pekee, kutaniko fulani lilipanga kuhubiri Jumamosi na Jumapili jioni, na Jumatano na Ijumaa jioni. Kutaniko hilo lilipanga pia kuhubiri eneo la kibiashara. Wengi walifurahia kuhubiri wakati huo hivi kwamba kutaniko likaamua kuendelea na mpango huo.
5 Fanya Ziara za Kurudia kwa Bidii: Ikiwa ni vigumu kuwapata watu nyumbani unapofanya ziara za kurudia, kila wakati unapowatembelea jaribu kufanya mpango hususa wa kurudi. Kisha hakikisha umerudi kama ulivyoahidi. (Mt. 5:37) Inapofaa, unaweza kumwomba mwenye nyumba namba yake ya simu ili uweze kuwasiliana naye tena.
6 Bila shaka, Yehova atabariki jitihada zetu za kuwatafuta wanaostahili na kusitawisha upendezi wao.—Met. 21:5.